- Wakili huyo alikatwa mikono na afisa wa polisi Nancy Njeri
- Uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo
Wakili mmoja aliyekuwa akihudumu huko Makueni ambaye mikono yake ilikatwa na afisa wa kike wa polisi ameaga dunia .
Onesmus Masaku aliaga dunia siku ya jumapili katika hospitali kuu ya Kenyatta ambako alikuwa akipokea matibabu baada ya shambulizi hilo nyumbani kwake Wote na polisi constable Nancy Njeri.
Mwenyekiti wa chama cha LSK tawi la kusini mashariki Justus Mutisya amesema Msaku aliaga dunia mwendo wa saa sita mchana .
Masaku alikuwa aelazwa katika hospitali ya rufaa ya Wote baada ya shambulizi hilo na baadaye kuhamishwa hadi katika hospitali ya KNH . Alikuwa akiuguza majeraha ya mkono baada ya mikono yake kukatwa . Mutia amemtaka Masaku kama mtu aliyekuwa na bidii na kifo chake kwa ghafla ni jambo ambalo limewashtua wenzake .
Afisa wa Polisi Nancy Njeri wa kituo cha Polisi cha Makueni hajafikishw akortini huku polisi wakisema uchunguzi unaendelea .
Suala hilo litatajwa tarehe 23 oktoba baada ya polisi kuitisha muda wa siku 14 zaidi kukamilisha uchunguzi wao.