Muundo Mpya wa Serikali

Muundo mpya wa serikali endapo ripoti ya BBI itapitishwa

Serikali kurejeshwa bungeni

Muhtasari
  •  Rais atakuwa na naibu wake 
  • Waziri mkuu atakuwa na manaibu wawili 

 

Rais Uhuru Kenyatta

Ripoti ya BBI  ambayo imekuwa mada katika ndimi za wengi katika siasa hatimaye imetolewa na mapendekezo yake makuu kudhihirika .

 Ripoti hiyo ilikabidhiwa kwa rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga  katika hafla iliyoandaliwa huko Kisii .

 Kabla ya  ripoti hiyo kutolewa  wanasiasa wamedai kwamba  ililenga kuvuruga   azma ya baadhi ya viongozi wa kisiasa nchini  au kuunda nafasi kuu za uongozi kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022 .

 Ripoti hiyo imebadilisha pakubwa muundo wa serikali na bunge  b na endapo itapitishwa  serikali itapanuliwa ili kuwa na waziri mkuu na manaibu wake wawili .waziri mkuu atakuwa na maamlaka huku mawaziri wakitarajiwa kuteuliwa kutoka kwa wabunge .

 Katika ripoti hiyo  kundi hilo  limependekeza kurejeshwa kwa serikali katika bunge ambapo  nafasi za waziri mkuu ,manaibu wawili wa waziri mkuu ,mwanasheria mkuu na kiongozi  wa upinzani

 Muundo huo ni tofauti  na tulicho nacho sasa ambapo  rais anasaidiwa na naibu wake .

 Upanuzi huo  wa serikali unalenga kuhakikisha kwamba jamii  zote zinajumuishwa katika serikali ili kuepuka mtindo wa sasa  ambapo mshindi huchukua yote .

 Chini ya mapendekezo ya kamati hiyo  serikali itakuwa na rais  ,naibu wa rais ,waziri mkuu ,manaibu wawili wa waziri mkuu  na mawaziri .

 Mapendekezo hayo sasa yatatosheleza  matamanio ya rais Kenyatta na kiongozi wa ODM  Raila Odinga  kuafikia malengo yao chini ya mwafaka wa Handshake ambao walisaini machi mwaka wa 2018

 Raila amekuwa  akisisitiza kwamba  muundo wa serikali uwe kama mapendekezo yaliyokuwa yametolewa katika katiba ya Bomas .

 Katiba ya Bomas ilikuwa imependekeza kuundwa kwa afisi ya  rais ambaye ni  kiongozi wan chi ,kamanda mkuu wa majeshi  na mwenyekiti wa baraza la kitaifa la usalama .

 Kulingana na kamati hiyo ,badala ya kuwa  na mfumo wa sasa wa urais ,kutakuwa na muundo unaojumuisha afisi ya rais na bunge .