- BBI inataka ipoa kuwa maamlaka huru
- Idara za magereza polisi wa utawala na huduma ya polisi zitawekwa chini ya usimamizi wa IG
Mwenyekiti wa Mamlaka ya kusimamia shughuli za polisi IPOA Anne Makori amekaribisha mapendekezo yaliyomo katika ripoti ya BBI ya kuibadilisha IPOA kuwa Mamlaka .
Makori amesema iwapo mapendekezo hayo yatapitishwa itakuwa rahisi kwa majukumu ya IPOA kuzidishwa ili pia kusimamia idara nyingine za usalama na sio Huduma ya polisi pekee .
Hatua hiyo inamaanisha kwamba kupitia marekebisho ya sheria bungeni Ipoa itaweza kuzisimamia idara kama vile Magereza ,KWS NA Shirika la kulinda Misitu nchini KFS .
Ili kuhakikisha kwamba polisi wanawajibika katika utendakazi wao BBI inalenga kuibadilisha IPOA kuwa mamlaka huru ili kuwachukulia hatua polisi wanaokiuka mikataba ya utendakazi wao
Makori amesema mapendekezo hayo ya BBI yanaipa mwamko mpya IPOA . Pia mapendekezo hayo yanaziweka idara za polisi wa utawala ,magereza na huduma ya polisiu chini ya Inspekta mkuu wa polisi .