Ruto Mashakani Bomas

'Heshimu rais!: Ruto akemewa na wajumbe Bomas wakati akieleza baadhi ya mambo anayotilia shaka katika BBI

Alikuwa akieleza baadhi ya mambo anayopinga

Muhtasari

 

  •  Ruto amesema idara ya mahakama inafaa kuwa huru 
  • Amesema Polisi  hawafai kuingiliwa na wanasiasa 
  • Alionekana kuendeleza msimamo wake kuipinga ripoti ya BBI 

 

Naibu wa Rais William Ruto

 Naibu wa rais William Ruto  siku ya jumatatu  amejipata pabaya wakato hotuba yake kuhusu mambo yanayofaa kubadilishwa katika ripoti ya BBi ilipowakera baadhi ya wajumbe .

 Watu waliokuwa katika ukumbi huo walianza kumtaka Ruto kumheshimu rais  . Ruto alikuwa ameratibu baadhi ya mambo yaliofaa kubadilishwa ama kuboreshw akatika ripoti hiyo ya BBI .

 Ruto alisema kwamba kuteuliwa kwa afisi ya  tume ya mamalamishi ambayo mkuu wake atateuliwa na rais ni kuingilia uhuru wa idara ya mahakama .

Ruto  alisema hatua hiyo inaweza kulirejeha taifa katika siku za kale  ambapo  rais alikuwa akitoa maelekezo kwa majaji kupitia  simu . Ruto amesema wakenya wengi wangali wanapata ugumu kuafikia haki  na baadhi ya masuala hayo yanafaa kushughulikiwa na katiba . Ruto amesema idara ya mahakama inafaa kupewa ufadhili wa kutosha .

Ruto  alikosoa pia pendekezo la kuvitaka baadhi ya vyama vya kisiasa kuwateua makamishna wa uchaguzi . Alijaribu kumpa Raila Odinga mfano kutumia soka akisema mchuano hauwezi kuwa na usawa endapo baadhi ya timu zitaruhusiwa kuwateua  marefarii . Raila hata hivyo alionekana kutozingatia ukosoaji huo wa Ruto na kuangalia kando