- 'Najua mama alikubali babangu Raila ako hapa tayari kuchukua mahari'
- Alikuwa akizungumzia matamshi ya wiki jana ya rais Kenyatta alipokuwa ziarani Kisumu ambapo alisema kwamba anazingatia kumtafuta mke wa Pili kutoka eneo hilo
Kulikuwa na ucheshi katika ukumbi wa Bomas wakati mwakilishi wa watu wenye ulemavu wa kuongea Ashura Michael alipotoa posa kwa rais Uhuru Kenyatta
"Mheshimiwa Rais recently you went to Kisumu na nikasikia ulikuwa unatafuta mpango wa kando. Najua mama alikubali babangu Raila ako hapa tayari kuchukua mahari na ndugu yangu deputy president akikubali atakuwa bestman," Ashura alisema kwa utani
Aliongeza kusema ;
.."Na mama wa taifa tutaendelea kubuild bridges pamoja. Na sasa mtoto wa BBI atazaliwa.
Usemi wake uliwachangamsha wote katika ukumbi huo walioangua kicheko huku raus Uhuru akimgeukia Raila na kupiga makofi naye naibu wa rais William Ruto akionekana pia kufurahishwa na utani wa Mrembo huyo .
Alikuwa akizungumzia matamshi ya wiki jana ya rais Kenyatta alipokuwa ziarani Kisumu ambapo alisema kwamba anazingatia kumtafuta mke wa Pili kutoka eneo hilo
"Nilikuwa naambia Raila hapa jameni... Sijui kama mama nyumbani ataniruhusu... Akiniruhusu labda naweza kupata mtu ambaye atakuwa ananitengenezea mambo yangu pande hii..." Alisema katika hotuba yake
"Ndio tuwe tukitembea ukijua kuna mahali utakuwa unakula ugali ama namna gani