Mos mos..2022 itafika

Kuja pole pole! Uhuru amfanyia Utani DP Ruto Kuhusu kampeni za 2022

Uhuru amesema Ruto alianza kukimbia akielekea upande wa pili

Muhtasari
  •  Rais  alishangaa mbona Ruto ameanza kampeini za mapema 
  •  Ruto na  Rais walionekana wakicheka kuhusu kijembe hicho cha Uhuru 
  •  Uhuru amesema vijana hawafai kuchochewa bali kuhusishwa katika maaamuzi 

 

Rais Uhuru Kenyatta ameonekana kueleza taswira  ilivyo kati yake na naibu wake William Ruto kuhusu uchaguzi wa mwaka wa 2022 . Uhuru alionekana kutumia hafla ya uzinduzi wa ripoti ya BBi kutoa maoni yake kuhusu kinachoonekana na wengi kama hatua ya Ruto kuanza kampeni za mapema za uchaguzi huo .

Uhuru amesema haelewi jinsi naibu wake alisahau kuhusu malengo yao ya Jubilee na kuanza kampeini za uchaguzi huo . Alitoa mfano wa mbio za kupokezana vijiti akisema  mwanarioadha anafaa kumpa mwenzake kijiti aendelee kukimbia lakini naibu  wake ‘amepinduka na kuanza kukimbia akirudi upande ule mwingine’ matamshi ambayo yalizua kicheko katika ukumbi wa Bomas

"Tulisonga pamoja lakini hapa kati kati ndio sasa 2022 ikaingilIa akasahau yale mengine but nasema tutulize boli..’ Uhuru amesema

"2022 itakuja  miaka  hairudi nyuma.. Tuko relay, lakini sasa my brother William anapinduka anakimbia nyuma..mos mos.. utafika tu’ Uhuru alisema huku akicheka

  Wakati rais alipokuwa akicheka  Ruto  aliamka kumueleza kitu cha utani na rais akazidi kucheka naye Ruto akirejea katika kiti chake .

Ruto  alijipata katika hali  isiokuwa nzuri wakati baadhi ya wajumbe katika ukumbi wa Bomas walipoana kumkemea akieleeza mambo ambayo anayapinga kaika ripoti ya BBI .

 Uhuru aliendelea na hotuba yake akisema kwamba ‘hatufai kukubali sarakasi  ambazo zinaizuia Kenya kufaulu’

" Naamini tunaweza  kuafikia mengi na kuipya changamoto hii . tunajifanya sisi ni viongozi wa kitaifa  lakini wakati unawpofika tunaanza lugha za mama ….’

Uhuru pia alieleza jinsi suala la vijana linafaa kushughulikiwa vizuri na kwa njia ya ustadi

"... Sio kwa kuwachochea lakini kwa kuwahusisha katika mchakato wa kufanya maamuzi’ alisema rais

" Iwapo tunataka kushughulikia tatizo la vijana kwana tushughulikie uchumi wetu .hakuna uchumi unaostawi kwa kipindi cha miaka mitano ya kisiasa’