Kifo

Mwalimu Mkuu wa shule ya Upili ya Tononoka afariki kwa ajili ya Covid 19

Alikuwa miongoni mwa walimu 11 waliopatikana na Covid 19 katika shule yake

Muhtasari

 

  • Mwalimu huyo alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mombasa kwa siku 11 zilziopita  na alizikwa mwendo wa saa tisa alasiri
  •  Shule zote mbili za  Star of the Sea  na Tononoka secondary zimefungwa . Masomo hata hivyo  yameendelea katika shule ya upili ya Mama Ngona licha ya visa kuripotiwa

 

 

Mwalimu mkuu wa shule ya upili ya Tononoka  Moahammed Khamis ameaga dunia kwa ajili ya Covid 19 /Kifo chake kinairi siku moja tu baada ya shule hiyo kufungwa kwa ajili ya ripoti za kusambaa kwa ugonjwa huo katika shule ya Tononoka .

 Naibu wake  Benjamin Kitsao Nzaro  amethibitisha kicho cha mkuu wake akisema marehemu alikuwa amelazwa hospitalini mjini Mombasa  wiki jana .Ameaga dunia jumatatu alasiri .

 Mwalimu huyo alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mombasa kwa siku 11 zilziopita  na alizikwa mwendo wa saa tisa alasiri .

 Masomo katika shule mbili za upili huko mombasa  yalikatizwa wiki  jana baada ya walimu 15 kuambukizwa virusi hivyo  .

 Kamishna wa kaunti ya Mombasa Gilbert Kitiyo  alisema walimu 11 kutoka shule ya upili ya Tononoka na wanne  kutoka Mama Ngina High School walipatikana na vrusi vya corona .

Kitiyo amesema sampuli  zimechukuliwa kutoka kwa waloimu wa shule ya upili ya Star of the Sea baada ya kuripotiwa kwa visa vya ugonjwa huo katika shule hiyo .

 Shule zote mbili za  Star of the Sea  na Tononoka secondary zimefungwa . Masomo hata hivyo  yameendelea katika shule ya upili ya Mama Ngona licha ya visa kuripotiwa

 Afisa mkuu wa afya wa kaunti ya Mombasa  Pauline Oginga  amesema usimamizi wa shule  ya Star  of the sea   ilikuwa imetaka kuchukuliwa kwa sampuli ili zifanyiwe vipimo .

Waziri wa elimu George Magoha ameonya  dhidi ya kufunguliwa kwa shule baada ya watu 931 kupatikana na virusi hivyo siku ya jumapili . Akizungumza mjini Nairobi  Magoha amesema baraza la mawaziri halijaidhinisha uamuzi wa shule zote kufunguliwa .