BBI

Murkomen amshutumu Uhuru kwa kuligawanya taifa kupitia BBI baada ya mkutano wa Naivasha

Murkomen akosoa mkutano wa Naivasha

Muhtasari
  •  Murkomen amesema rais anafaa kuzungumza na viongozi wote 
  •  Amedai kwamba kuna njama  ya kuitumia BBI  kuwagawanya wakenya 

 

Seneta wa Elgey Marakwet Kipchumba Marakwet

 

Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen amemshtumu rais Uhuru Kenyatta kwa kuigawanya nchi  kupitia mchakato wa siasa za BBI

 Kupitia twitter  seneta huyo amesema Uhuru anafaa kutumia maafikiano katika kuhakikisha kwamba mapendekezo ya BBI yanapitishwa bila kuzua mgawnayiko miongoni mwa wakenya .

"  Nataka kumrai rais Uhuru akome kuligawanya taifa . rais anafaa kuwa kiongozi wa wote  na kujifunza kuwanganisha wakenya  na sio hii dhana ya ‘utafanya nini’  Murkomen amesema

 Alikuwa akijibu  posti moja ya Ikulu kutangaza mkutano kati ya rais Uhuru Kenyatta a wabunge wanaounga mkono BBI  mjini Naivasha .

 Viongozi kutoka bunge na senate  wamekuwa wakikutana Naivasha  ili kujadili  masuala tata katika ripoti ya BBI .

 Washirika wa Uhuru na kiongozi wa ODM Raila Odinga wamekuwa wakiitisha kupitishwa  kwa ripoti hiyo bila marekebisho ilhali  washirika wa naibu w arais William Ruto wanataka baadhi ya mapendekezo hayo kujadiliwa na kufanyiwa marekebisho .

 Kauli yake  iliungwa mkono na mbunge wa Kikuyu  Kimani Ichung'wa,  aliyesema  kwamba  mchakato wa BBI  unatumiwa  kuwagawanya wakenya  ili kuafikia ajenda ya kisiasa