Hongera Biden

Uhuru, Raila wampongeza Rais Mteule wa Marekani Joe Biden

Rais na Odinga wamesema ushindi wa Biden utaboresha uhusiano kati ya kenya na Amerika

Muhtasari

 

  •  Rais Uhuru amesema  Wamarekani wametoa sauti yao kupitia kura 
  •  Biden amesema ni wakati wa kuiponya Marekani baada ya mgawanyiko wa kisiasa 
  •  Donald Trump amezidi kushikilia kwamba hajashindwa katika uchaguzi huo 

 

Rais Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa kumhongera rais mteule wa Marekani Joe Biden  kufuatia ushindi  wake katika uchaguzi wa Marekani .

Uhuru ametaja ushindi wa Biden kama  ishara ya wamerakani kuwa na matumaini na uongozi wa makamu huyo wa zamani wa rais .

" Wamerakani wamezungumza kwa sauti  kupitia kura zao  kwa kumchagua  kiongozi mwenye uzoefu mkubwa  kuwa rais wao’ amesema rais Kenyatta

" kwa niaba ya  watu na serikali ya Kenya namhongera Biden na makamu wake Kamala Harris  kwa ushindi wao  wanapojitayarisha kungoza Amerika…’

 Rais amesema Biden ni rafiki wa Kenya  ambaye ziara yake ya mwisho nchini ilikuwa akiwa makamu wa rais  wa  Barack Obama ilisaidia kuimarisha uhusiano  kati ya Kenya na Marekani

 Rais  alimhongera Harris kwa kuandikisha historia baada ya kuwa mwanamke wa kwanza kushikilia nafai hiyo ya pili  ya uongozi nchini Marekani .

 Kwa upande wake kiongozi wa ODM Raila Odinga  pia alimhongera Biden  kwa ushindi wake  akisema Kenya inangoja kushirikiana naye atakapoanza kuiongoza Marekani

" Tunatarajia  kushirikiana kuhusu  changamoto kubwa za ulimwenguni ikiwemo kukabiliana na corona,kudorora kwa uchumi  na mabadiliko ya hali ya  hewa.Kila la heri’ amesema Odinga .

Biden amesema ni wakati wa ‘kuiponya’ Amerika katika hotuba yake ya kwanza baada  kutangazwa kuwa mshindi  siku ya jumamosi  huku rais Donald Trump akikataa kukubali matoeo na kupa kupinga matokeo yalimweka Bden kileleni kupitia kesi mahakamani  .