DPP amesema kwamba idadi ya watuhumiwa wanaopatikana na makosa mahakamani ni mojawapo ya vigezo vinavyotumiwa kukadiria mafanikio ya kupambana na ufisadi .
" Tumeshuhudia ongezeko la idadi ya kesi ambazo watuhumiwa wamepatikana na hatia kwa asilimia 63.16 katika nusu ya kwanza ya mwaka wa 2020’
Idadi ya kesi zilizotamatika kwa watuhumiwa kupatwa na hatia zilikuwa 7, 27, 35, 43 na 45 mwaka wa 2015, 2016, 2017, 2018 na 2019 mtawalia
Kiwango cha kupatikana na hatia kilikuwa 30.4%, 46.55%, 37.63%,47.25% na 47.27% katika miaka ya 2015, 2016, 2017, 2018 na 2019 mtawalia " Haji amesema
Jumla ya kesi 26 zilisajiliwa kufikia juni tarehe 26 mwaka huu huku kesi 78 zikiripotiwa mwaka wa 2019 na kesi 116 zikiripotiwa mwaka wa 2018
Jumla ya kesi 238 zilikimilishwa huku 20 zikikamilishwa kufikia juni tarehe 30 mwaka huu ,kesi 103 mwaka wa 2029 na kesi 115 mwaka wa 2018