- Wanapatholojia M mwangi na Dr.P Maturi wamesema sampuli zilizokusanywa za DNA zimeonyesha kwamba Murunga alikuwa baba ya mtoto mmoja – wa kike
- Murunga aliaga dunia Novemba tarehe 14 alipokuwa akipelekwa hospitalini baada ya kuanguka na kuzirai akiwa nyumbani kwake
Sampuli za DNA zilizopimwa zimethibitisha kwamba marehemu mbunge wa Matungu Justus Murunga ndiye baba ya mmoja wa watoto wa mpenzi wake Agnes Wangui
Wangui alikuwa amedai kupitia stakabadhi za mahakama kwamba alikuwa amewapata watoto wawili na marehemu mbunge huyo . mmoja ni mvulana wa miaka saba na mwingine ni mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 3 .
Wanapatholojia M mwangi na Dr.P Maturi wamesema sampuli zilizokusanywa za DNA zimeonyesha kwamba Murunga alikuwa baba ya mtoto mmoja – wa kike
Vipimo vya DNA havikumhusisha mtoto huyo wa kiume .
Wangui na Murunga walifahamiana kwa miaka saba . walikutana mara ya kwanza mwaka wa 20212 wakati marehemu alipokuwa akifanya kazi katika shamba la Embakasi ilhali Wangui alikuwa mfanyibiashara katika eneo la Ruai .
Wakati huo huo wakili Danstan Omari jana amesema atawasilisha kesi kortini ili kuhakikisha mtoto huyo wa kiume pia ana haki ya kupata Uradhi kwa sababu alikuwa pia akimtegemea Marehemu Murunga .
Murunga aliaga dunia Novemba tarehe 14 alipokuwa akipelekwa hospitalini baada ya kuanguka na kuzirai akiwa nyumbani kwake