- Walifanya mazungumzo mafupi na Mutitu akamueleza kwamba alikuwa na nafasi katika jeshi aliotaka kumpa mtu ,hatua iliyotumiwa kumnasa mlalamishi na kumfanyoa atoe pesa zake .
- Mume wake Leonard alimuarifu Okemer kwamba mke wake ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi zima la usajili wa makurutu wa kujiunga na jeshi .
Mwanamme mmoja amewailisha kesi kortini baada ya jamaa zake wawili kumfanya uze shamba lake ili aweze kutoa hongo kupata kazi feki ya KDF .
Leonard Etyang Okemer amesema alidanganywa kuuza shamba lake huko Teso kwa na kuwapa walaghai shilingi milioni moja . Richard Ouma Okemer na Lucy Catherine Mutitu walishtakiwa kaika mahakama ya kibera kwa ulaghai huo .
Pia walishtakiwa kwa kujifanya kuwa maafisa wa KDF kinyume cha sheria na kupokea fedha kutumia wongo .
Uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba Mutitu ameolewa na binamu ya mlalamishi . Wakati mlalamishi alipokutana naye alijitambulisha kwake kama afisa wa KDF anayehudumu Garissa .
Walifanya mazungumzo mafupi na Mutitu akamueleza kwamba alikuwa na nafasi katika jeshi aliotaka kumpa mtu ,hatua iliyotumiwa kumnasa mlalamishi na kumfanyoa atoe pesa zake .
Mume wake Leonard alimuarifu Okemer kwamba mke wake ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi zima la usajili wa makurutu wa kujiunga na jeshi .
Leonard kisha alielekea Teso na kujifanyakuchukua picha za boma la mlalamishi huku akimuambia kwamba tayari alikuwa ameshamuingiza katika jeshi .
Alisema sehemu ya fedha hizo zilikuwa za kununua sare za jeshi , dawa ,bunduki za kufanya mazoezi na risasi . Mwanamme huyo aliuza shamba lake na kumpa shilingi 850,000 kisha mshukiwa akatoweka .
Uchunguzi ulianzishwa na Mutitu akakamatwa na kushtakiwa septemba mwaka jana .Alikana mashtaka dhidi yake mbele ya hakimu mkuu wa kibera Philip Mutua .
Siku ya jumanne Richard Okemer alishtakiwa na makosa ya kuchukua pesa kutumia wongo na kukana mashtaka hayo .
Kesi hiyo itatajwa jumatano ijayo ambapo itaunganishwa na ile ya Mutitu na pia mahakama itaamua kuhusu kuwaachilia washukiwa kwa bondi .