- Siku ya jumanne Odinga alifanya mkutano na wenyeviti wa matawi yote ya ODM kutoka kaunti zote katika makao makuu ya chama Chungwa House .
- Aliwaambia viongozi hao kwamba ODM itakuwa na mgombeaji wa urais na kutawaka wajitayarishe kwa kipute kikubwa ambacho alikitaka kama ‘mama ya chaguzi zoite za urais’
Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga amefufua mkakati kabambe wa kuhaisha azama yake ya kuwa rais na kuthibitisha kwa mara ya kwanza kwamba atawania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao .
Chama hicho kimeanzisha kampeini ya mashinani ili kumtangaza Raila akama anayefaa kumrithi rais Uhuru Kenyatta atakapokabiliana na naibu wa rais William Ruto katika kipute hicho kikali .
Chama hicho kinalenga kufufua matawi yake yote 47 kote nchini ili kuleta uchangamfu miongoni mwa wafuasi wa Odinga na kujaza nafasi za viongozi walikihama ODM na kujiunga na vyama vingine .
Siku ya jumanne Odinga alifanya mkutano na wenyeviti wa matawi yote ya ODM kutoka kaunti zote katika makao makuu ya chama Chungwa House .
Aliwaambia viongozi hao kwamba ODM itakuwa na mgombeaji wa urais na kutawaka wajitayarishe kwa kipute kikubwa ambacho alikitaka kama ‘mama ya chaguzi zoite za urais’
Katika mahojiano na gazeti la The Star ,maafisa wakuu wa ODM na walio karibu na Raila wamethibitisha kwamba Raila atakuwa katika debe katika ari yake ya kutaka kumrithi rais Uhuru Kenyatta .
“ Tumeanzisha shughuli zetu .mtu yeyote anayefikiri kwamba hatupo katika kinyang’anyiro hiki anafaa kujua kwamba tupo’ amesema mwenyekiti wa ODM John Mbadi .
Hatua hiyo sasa huenda ikapunguza kipute hicho cha mwaka wa 2022 kuwa makabilianao makali kati ya Raila na Ruto .
“ Kando na BBI ,Raila atakuwa akiwania urais 2022.Atakuwa na shughuli nyingi katika siku zijazo’ amesema Mbadi .
Kampeini za Raila zitategemea ujumbe wa mkataba wake wa kuiunganisha nchi na rais Uhuru Kenyatta kupitia mwafaka wa BBI .