Winfred Nduku baadaye alijaribu kujiua kwa kujidunga kisu tumboni lakini majirani walifaulu kumuokoa. Polisi na majirani wanasema mshukiwa alirejea nyumbani usiku na kisha kuanza kugombana na mamake kuhusu kuwalisha watoto hao. Kwa sababu ya hasira alichukua kisu na kuwadunga watoto wake wawili walio na umri wa miaka miwili na saba. Polisi waliipata miili ya Amina Nduku na Jamil Kilonzo ikiwa imelowa damu .
Walipelekwa katika hospitali iliyo karibu ambako walitangazwa kuaga dunia. Mama yao alikimbizwa katika hospitali ya mama Lucy na kulazwa, hali yake ikiwa thabiti. Nyanya ya watoto hao amesema yeye na binti yake walikuwa wakigombana kuhusu chakula cha watoto hao. Mkuu wa polisi Nairobi Philip Ndolo amesema polisi wanamngoja Nduku apone kabla ya kumhoji kwa lengo la kumshtaki kwa mauaji .