Peter kabla ya kifo chake alikuwa katibu mkuu wa kanisa la Presbyterian Churches of East Africa (P.C.E.A), na kuaga kwa ajili ya virusi vya corona.
Akizungumza wakati wa hafla ya mazishi hayo alisema kuwa alikuwa amempeana mwanawe kwa Mungu na alitenda alichokuwa amepanga Mungu.
"Kania mwanangu nakumbuka vile ulikuwa mchanga na vile umekua kwa immani, nilikulea na kukupeana kwa Mungu ili umtumikie, sina hisia mbaya kwa maana umefarikiUlinipenda na ukanisadia kwa vyovyote vile nilivyokuwa nahitaji, ulihakikisha nimeishi maisha mema, marafiki wako wote wamekuwa wanangu kwa maana uliwatambulisha kwangu
Familia yako ulioacha nyuma, Mama Njeri,Njeri,Kariuki na Joel sasa ni wanangu Moyo wangu umepumzika kwa kujua uko na mwenyezi Mungu." Alizungumza.
Pia alimshukuru kwa kumuachia watumishi wa Mungu, amabo watamlinda wakati hayupo tena,
"Nina shukrani nyingi kwa kuniachia watumishi wa Mngu kama Reverend Caro watakao nilinda kama huyuko, najua siyuko pekeyangu siana maneno yakutosha ya kunakili kueleza jinsi nimehuzunika siku hii ya leoUpendo wa amamkwa mwanawe huna mwisho, huwa unakua na unakua na unazidi kukua hata baada ya kifo, mwanangu umepigana vita vyema
Umemaliza mbio zako umekaa na imani(2 Timotheo4:7) lala salama mwanangu, tutapatana tena mbinguni kwa maana hapo ndipo tunaelekea."