Soma hapa:
"Kitambulisho kinasema mimi ni Andrew Mbugua. ID na passport zinaonyesha mimi ni mwanaume . Nikitoa pesa kwa Mpesa huwa wananiuliza madam mbona ID yako inasema wewe ni mwanaume." alisema Audrey.
Audrey anasema kuwa wazazi wake huwa wanachanganyikiwa na hali yake na kumuita kama mwanamme.
"Sometimes huwa wananiita "He'....babangu na mamangu hawajazoea kuniita "She". Alisema Audrey.
Audrey anasema kuwa ilimbidi akaacha hasira na kukubali hali yake.
"Kuwa na machungu mengi ni mimi nitaumia. Ni mimi nitakuwa na presha."
Soma hapa:
Audrey anaeleza kuwa kuna utaratibu wa kufuata katika kubadilisha jinsia kwenda nyingine. Juhudi za Audrey ziligonga mwamba wakati madaktari walisema wanahitaji wazazi wake ili waweze kuidhinisha upasuaji.
"Sikuweza kupata uwezo wa kubadilisha sehemu zangu nyeti. Viongozi walitaka idhini ya wazazi ili kubadilisha sehemu zangu nyeti. Hauhitaji ruhusa kugeuzwa vitu pale chini." Alihoji Audrey.
Audrey aliwahi kupata ushindi kupitia mahakama kuu ili kupata vyeti vyake vya shule kubadilishwa jinsia na jina lake.