Idadi ya visa vya COVID-19 Uganda vyaongezeka maradufu, 84 wapatwa na virusi

954916307fcd1bd2
954916307fcd1bd2
Uganda imerekodi idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya corona huku wagonjwa 84 wakiugua na kupelekea idadi jumla katika taifa hilo la Afrika Mashariki kuwa 413.

Katika visa hivyo 84, visa 52 ni madereva wa trela ambapo 50 wao waliwasili kutoka Sudan Kusini kupitia Elegu, huku wengine wawili wakitokea Kenya kupitia Busia na 32 walikuwa karantini.

Kwenye taarifa kupitia Twitter, Waziri wa Afya wa Uganda mnamo Jumamosi, Mei 30, alisema madereva 51 ambao walipatwa na ugonjwa huo walirejeshwa katika mataifa yao.

https://twitter.com/MinofHealthUG/status/1266850318370947072

Kufikia sasa taifa hilo lina watu 71 waliopata nafuu ambao waliondoka hospitalini kote nchini. Katibu Mkuu katika Wizara ya Afya, Diana Atwine alionyesha hofu yake kuwa idadi ya waliotangagusana na madereva wa lori huenda inasambaza ugonjwa huo kwa sababu bado wengine wao hawajaweza kufikiwa.

Inadaiwa kwamba mgonjwa mmoja asiyeonyesha dalili za COVID-19 anaweza kusambaza ugonjwa huo kwa zaidi ya watu 80.

Taifa hilo linaongozwa na Rais Yoweri Museveni lilikuwa limedokezea kwamba linapania kuondoa sheria ya kutotoka nje kuanzia Juni, lakini kuongezeka maradufu kwa idadi ya maambukizi ni changamoto kubwa ambayo huenda hatua hiyo ikasitishwa.

Kiongozi wa taifa anatazamiwa kuhutubia taifa hilo mnamo Jumatatu, Juni 1, ili kutoa maelekezo zaidi ya nini kitafuata kuhusiana na kuondolewa kwa sheria ya kutotoka nje.

Museveni alikuwa ameamuru kwamba itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuvalia vitamvua punde shughuli za uchumi zitafunguliwa. Serikali iliahidi kutoa maski za bure kwa wananchi na wale ambao watapatikana hawajavalia watakamatwa.