Mipango ya Harusi yake JB Masanduku inayotarajiwa kufanyika tarehe 11 mwezi Novemba imekamilika na mambo yote yako seti.
Hata hivyo, harusi hio ilifaa kufanyika tarehe 24 mwezi wa nane siku ya kuzaliwa ya mpenziwe Jackie Karanja lakini sasa itafanyika tarehe 11 mwezi Novemba siku aliyoaga dunia mamaye mzazi.
"Hii ni siku spesheli ya mamangu mzazi na ningependa sana kumpa heshima zake huku pia nikitaka kumfurahisha mpenzi wangu,"Alisema JB masanduku. JB pia anasema kuwa mpenziwe angetamani sana kumuona mamaye mzazi aliyeiaga dunia.
"Nimezungumza na watu wangu na wakanihakikisHia kuwa mambo yote yapo tisti. Mke wangu aliamua kumpa heshima mamangu kwa kuichagua siku aliyoniacha mama."
JB anamesema kuwa mamake mzazi alimsaidia kuwa na uulivu kila wakati kwani alijua kuwa haraka haraka haina baraka. Kwenye harusi yake, JB amewaalika watu mashuhuri huku naibu rais akiwa wakwanza kukubali wito wake.