Dhamira kubwa ya kuwateua watalaam kuhudumu kama mawaziri ilikuwa kuhakikisha kwamba wanatekeleza majukumu yao kikamilifu bila muingilio wa kisiasa lakini hilo limekosa kuzaa matunda kwani utendakazi wa mawaziri watalaam haujaweza kuisadia serikali kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi . Wadadisi pia wanaamini kwamba hatua kuwanyima wabunge fursa ya kuwa mawaziri ndio hatua inayofaa kulaumiwa kwa hamu yao ya kutaka kuongezwa mishahara na kujiongeza marupurupu kila mara.
Wanaounga mkono hatua ya kuwateua wabunge kuwa mawaziri wamesema hatua hiyo itaiwezesha serikali kuokoa fedha kwani haitawalipa mawaziri na wabunge ila mbunge anayeteuliwa kuwa waziri ataongezwa takriban shilingi laki nne kwa mshahara wake wa sasa kama mjumbe .Pia wanasema pesa zinazotumiwa kuwalipa wafanyikazi wa mawaziri wa sasa ,magari na marupurupu zitaweza kuokolewa endapo wabunge wataweza kuteuliwa kuwa mawaziri . Je unaunga mkono pendekezo la kuwateua wabunge kuwa mawaziri?