Mwanamume wa umri wa miaka 30 ameshtakiwa kwa kutekeleza tendo lisilo la kawaida na mtoto. James Wasike anadaiwa kumlazimisha mtoto wa miaka 12 kumbusu na kumgusa sehemu zake za siri akiwa nyumbani kwake Julai 22.
Pia anadaiwa kumvua nguo mtoto huyo na kumpapasa sehemu zake nyeti.
Mtoto huyo alikuwa ametumwa na mamake kuchukua pesa kutoka kwa rafikiye na ndipo Bwana Wasike alipomlazimisha kwenda nyumbani kwake.
Wasike alijaribu kumziba mdomo asipige kelele wakati alipokuwa akimvua nguo na hapo majirani wakavunja mlango na kumwezesha mtoto hyo kutoroka na Wasie akakamatwa. Hata hivyo amekana mashtaka na kuachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki tatu.