Mwakilishi maalum wa AU Kuhusu miundo msingi Raila Odinga alirejea nchini siku ya Jumapili usiku baada ya kufanyia upasuaji mdogo Dubai.
Raila aliwasili nchini mwendo wa saa nne usiku Jumapili. Ndege yake ilitua katika uwanja wa JKIA usiku, afisa mmoja wa usalama ameliambia gazeti la The Star.
Afisa huyo hata hivyo hakuweza kutoa maelezo zaidi kwa sababu ya utaratibu na itifaki. Star imethibitisha kwamba ndege hiyo mwanzo iliratibiwa kwenda Lusaka lakini ikaelekezwa kutua Nairobi.
Kiongozi huyo wa ODM Julai Mosi aliwashukuru wakenya kwa kumuombea apate afueni ya haraka baada ya kupokea matibabu katika Miliki za kiarabu, UAE.