Maafisa wawili wa IT waliowapiga picha ais Uhuru na Raila CBD washtakiwa

WASHUKIWA
WASHUKIWA
Maafisa wawili wa IT wanaofanya kazi  katika hoteli ya Stanley sarova  wanaitafuta taarifa ya rais Uhuru Kenyatta katika kesi ambayo  wameshtakiwa kwa kuzichukua picha za CCTV zilizowaonyesha viongozi hao wawili wakifika katika barabara ya Kenyatta Juni tarehe 2

Wakili wao  Danstan Omari  siku jumatano  amesema pia watamtaka kiongozi  wa ODM Raila Odinga kutoa taarifa . Raila na Uhuru walinaswa katika picha hiyo ya Video wakizuru miradi mbali mbali inayoetekelezwa CBD .

Omari  amesema  wateja wake watazitumia taarifa hizo kama utetezi kwani wamepoteza kazi zao kwa ajili ya kesi hiyo .

Patrick Rading  na Janet Magoma  walifikishwa kortini jumatano na kushtakiwa kwa kukiuka sharia za kutumia vibaya komputa na uhalifu wa mtandaoni .

Omari  amemuambia hakimu Bernad Ochoi kwamba wateja wake hawakukiuka sharia yoyote kwani walikuwa tu wanaonyesha ‘uzalendo’

Inadaiwa wawili hao  mwendo wa saa mbili na dakika 20 juni tarehe 2 waliichukua picha hiyo ya video  iliyowaonyesha rais Kenyatta na   msafara wae katika barabara ya Kenyatta .

Serikali haikupinga kuachiliwa kwao kwa  dhamana  na kuutaka upande wa utetezi  kutoa ushahidi  wa kuonyesha kwamba wateja wao wamepoteza kazi zao .

Waliachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu kumi pesa taslimu