Mabaki ya watu 28 waliofariki katika ajali ya ndege ya Ethiopia yawasili

Ndege iliyobeba mabaki ya Wakenya 28 walioangamia  kwenye  ajali ya ndege ya Ethiopia ilifika JKIA Jumatatu asubuhi.

Takribani Wakenya 32 walikuwa wameabiri  ndege  ya Boeing 737-Max wakati wa janga la Machi 10, ambalo liliwauwa abiria  wote157.

Familia za wahasiriwa wa ajali hiyo zilikuwa JKIA mapema asubuhi wakisubiri  kukabidhiwa mabaki hayo ya jamaa zao.

Ripoti ya awali iliyotolewa mnamo Aprili ilionyesha kuwa marubani  wa Ethiopia Airlines walipambana na mfumo wa kompyuta ambao uliamuru ncha ya mbele ya ndege kutazama chini kwa sababu ya data mbaya ya sensa.

Mfumo  huo  wa  sensa ya Kopmyuta ulitajwa  kusababisha ajali nyingine ya ndege katika Indonesia, ambayo iliwauwa watu 189.

Familia ya wahasiriwa ya  Kenya ilikuwa imewasilisha mashtaka huko Chicago mnamo Aprili dhidi ya kampuni hiyo ya ndege ya Marekani, Boeing  737-max8 kwa ajali hiyo.

George Kabau alisema anataka kulazimisha kampuni hiyo kutoa hati na barua pepe zinazohusiana na mfumo wa ndege ya 737 MAX 8, ambayo ilitengenezwa ulimwenguni pote baada ya ndege kuu mbili kuanguka nchini Ethiopia na Indonesia.

Mnamo Julai, Kenya iliambia Bunge la Marekani kwamba Boeing ilikuwa bado  haijaomba msamaha wa kibinafsi kwa familia za wale walioathiriwa.

Lakini kwa kuzingatia Mkataba wa Montreal, kila familia ya wahathiriwa wa ajali ya ndege hiyo inafaa kupokea kitia cha shilingi milioni 17.

Mkataba huo, uliopitishwa na Shirika la Kimataifa la ndege, unasema kwamba "ikiwa ndege itapatikana  na kosa kwa kusababisha ajali, kila abiria aliyeathiriwa atapata thamani isiyopungua $ 113,100.