Magavana wamtetea Oparanya kuhusu uamuzi wa kusistisha huduma za kaunti

Gavana wa  Makueni Kivutha Kibwana  na mwenzake wa west Pokot  John Lonyan’gapuo wamejitokeza kumtetea  mwenyekiti wa baraza la magavana Wycliffe Oparanya .

Wamesema sio haki kwa maseneta  kuanza kumshambulia  Oparanya kuhusu uamuzi wa kusitisha huduma katika kaunti zote kwa ajili ya ukosefu wa fedha ilhali hatua hiyo ilichukuliwa na baraza la magavana bali sio  na  oparanya pekee .

Wawili hao wamesema wafanyikazi wa kaunti wamekuwa wakifanya kazi kwa miezi mitatu bila malipo  na ni vyema iwapo watapumzika hadi walipwe pesa zao .

Oparanya akitangaza uamuzi huo siku ya jumatano amesema hatua hiyo imechukuliwa kwa ajili ya ukosefu wa fedha baada ya maseneta  kukoa kuafikiana kuhusu mfumo wa kutumiwa katika ugavi wa fedha kwa serikali za kaunti .

Alisema kwamba vituo vya afya vya kaunti havitawasajili wagonjwa wengine na vitatoa tu huduma adimu kwa wagonjwa wa kutibiwa na kurejea nyumbani huku wafanyikazi wa kaunti wakitakiwa kuchukua mapumziko ya   wiki mbili .

Oparanya amesema njia pekee ya kusuluhisha  tatizo hilo ni kwa hazina ya kitaifa kutoa fedha kwa serikali za kaunti haraka . Maseneta hata hivyo wameonakana kukerwa na uamuzi huo wa COG na kuanza kumshambulia Oparanya .

Baadhi ya maseneta wamemtaja kama msaliti huku wengine wakimuita mwongo  kwa kuongoza walicotaja kama kundi la ‘vijana’ wanaoshambulia bunge la senateambalo limekuwa likitetea kabisa ugatuzi .

Wamesema COG  chini ya uongozi wa oparanya imegeuzwa kuwa sehemu ya serikali kuu na kuisaliti senate ambayo imekuwa ikipagania mgao wa fedha Zaidi kwa serikali za kaunti .