Magoha aonya kuhusu ufisadi katika mradi wa madawati wa shilingi bilioni 1.9

magoha
magoha
Serikali imesema  haptakuwa na ulaghai katika mradi wa kutoa madawati kwa wanafunzi wa shule za msingi na upili .

Shilingi bilioni 1.9 zimetengwa kwa mradi huo  wa kutoa madawati kwa shule 15  za umma kwa kila kaunti ndogo  chini ya mpango wa kufumua cuhumi  kutumia madawati yanayotengezwa nchini .

Waziri wa elimu George Magoha  amesema kwamba  serikali imeweka mikakati ya kuzuia  ufisadi katika mradi huo wakati alipokuwa akitoa mwongozo wa jinsi utakavyotekelezwa kwa makamishna wa kaunti .

“ Huu sio wakati wa kuuliza ‘mimi nitanufaika vipi’ huu mradi ni wa watoto wetu’ Magoha amesema

Waziri Magoha aliongeza kwamba  shilingi bilioni1.9  zimetolewa chini ya mpango huo wa kufumua uchumi na unalenga biashara  ndogo ndogo na za wastani .

Ili pawepo uwazi  na kuepuka mapendeleo  katika mradi huo  serikali imetoa mwongozo utakaotumiwa  ambao huwatambua wanaonufaika na fedha za kila wiki za walioathiriwa na Covid 19 .

Katibu wa kudumu wa usalama wa ndani Karanja Kibicho  amesema ana matumaini  kwamba maafisa wa  utawala na serikali wataonyesha uadilifu katika  usimamizi wa mradi huo .

Mradi huo utapelekea madawati  622,367  na viti  yanatolewa kwa shule za umma  huku serikali ikiendelea kuweka mikakati kwa matayarisho ya kufunguliwa kwa shule .