Mapacha wawili wa Afrika Kusini wamuoa mke mmoja

mapacha wa afrika kusini
mapacha wa afrika kusini
Ni picha ambayo ili wekwa katika mtandao wa kijamii wa Twitter na Catchvibe Moatshe na mke wao wakiwa wamevalia mavazi ya jadi ya ngozi za wanyama.

Walikuwa wamezingirwa na jamaa zao na marafiki huku wakionekana walikuwa wamewaunga mkono katika hatua yao ya kumuoa mke mmoja.

Huku wananchi wa Afrika kusini wakitoa maoni yao kwa lugha ya kimombo katika mtandao ule. Zifuatazo ni baadhi ya jumbe ambazo waliweza kutuma kuhusiana na jambo hilo.

“When you're twins it doesn't automatically mean everything that you do in life should be the same," Ngoako aliandika

“Well, this is weird. What's weirder is I found out there is a thing called sologamy. It's a marriage by a person to oneself...”Tommyk aliandika katika mtandao.

“I'm better off with just whisky as my wife,” Alisema Gamroji

“This is not cool," Truth aliandika

“My question is when they have children how will they know which baby belongs to who. Hai, maybe they will play pick it, pick it, point I,” @tlou_makgaleng.

“I love twins soo much but these did an odd thing here These twins want to share everything Like literally,"@ Silokazie

“Lol... This is a joke, we are in the 21st century," Faris alisema

“Madness,” @NolenceMashego

“I have a lot of questions,” Lebogang aliandika katika mtandao huo.

Kilikuwa kisa cha kushangaza wengi kwa maana kisa kama hiki ambacho kimeshuhudiwa na wananchi wengi wa Kenya ni mwanaume kuoa wanawake wawili na wala si mwanamke kuolewa na wanaume wawili.

Mwaka uliopita Desemba 11 mwanaume mmoja kutoka Kajiado aliweza kuoa wanawake wawili katika harusi moja na siku moja.

Tom Mako almaarufu Jumior, 27,aliweza kumuoa Elizabeth Silamoi, 24, kutoka kijiji cha Enkorika na Joyce Tikoyian, 23, kutoka Empakasi karibu Kitengela.

Miaka miwili ilyopita Mako alipatana na Elizabeth akiwa amepeleka ng'ombe malishoni eneo hilo la Enkoria na kupatana pia na Joyce bado akiwa malishoni eneo la Empakasi,Kitengela.

Tikoyian aliweza kumaliza kidato cha 4 na silamoi aliweza kufika katika kidato cha 3.