Mapenzi tele! Orodha ya watu mashuhuri waliofunga ndoa zaidi ya miaka 25 iliyopita

Wiki hii mtangazaji wa kituo hiki Ghost Mulee alionyesha mapenzi kwa mkewe kwa kumpongeza kwa miaka 27 ya ndoa.Katika mtandao wake maridhawa wa Insta, Ghost aliposti picha yake pamoja na mkewe na kusifia ndoa yao.

"Mungu wa maajabu kweli. Miaka 27 imepata ila nahisi kama jana tu..." Alisema Ghost.

https://www.instagram.com/p/B6FOnjqFyY4/?utm_source=ig_embed

Kwa hilo tunaangazi orodha ya watu mashuhuri ambao waliofunga pingu za maisha zaidi ya miaka 25 na 40 zilizopita na mpaka sasa wanapendana si kidogo.

1.Barrack Obama na Michelle Obama

Aliyekuwa rais wa USA bwana Barrack Obama na mke wake Bi Michelle ni miongoni mwa wapenzi ambao wameishi katika ndoa zaidi ya miaka 25.

Wapenzi hawa waliooana mwaka wa 1992 walisherehekea ukumbusho wa miaka 27 wa harusi yao huku Michelle akimsifu mume wake kwa kutimiza yote aliyoahidi kufanya.

’27 YEARS AGO, THIS GUY PROMISED ME A LIFE FULL OF ADVENTURE. I’D SAY HE’S DELIVERED.

HERE’S TO OUR NEXT CHAPTER OF BECOMING EMPTY NESTERS AND DISCOVERING WHAT’S NEXT—WHILE STILL FEELING THE MAGIC THAT BROUGHT US TOGETHER ALL THOSE YEARS AGO. HAPPY ANNIVERSARY, BARACK. 💕’ Michelle alisema.

Obama naye hakuachwa nyuma. Alifunguka na kundika,

‘LIKE THE BEATLES SAID: IT’S GETTING BETTER ALL THE TIME. THANKS, BABE, FOR 27 AMAZING YEARS!’ 
2. Kathy Kiuna na Allan Kiuna

Waanzilishi wa Jubilee Christian Church mhubiri Kathy Kiuna na mume wake Bwana Alan Kiuna wameishi katika ndoa kwa miaka 25.

Wapenzi hawa wamebarikiwa na watoto watatu - mabinti wawili na kijana mmoja.

Hivi juzi, Kiuna aliandika ujumbe mtamu wa kumshukuru mke wake kwa kubaki naye hata wakati ambao kulikuwa na matatizo maishani mwake.

‘I WISH I COULD EXPLAIN HOW MUCH THE LIGHT IN YOUR EYES HAS SHONE IN MY DARKEST MOMENTS, I WISH I CAN TELL STORIES OF HOW YOUR SMILE HAS TRANSFORMED MY EMOTIONS IN MY TOUGHEST TIMES.

YOU HAVE TAUGHT ME THAT MARRIAGE IS NOT ABOUT THINKING ALIKE, BUT THINKING AS ONE AND REGARDLESS OF THE MANY TUNES LIFE HAS PLAYED ON US.

SOME HIGH AND OTHERS VERY LOW, YOU HAVE MADE A COMMITMENT TO ALWAYS DANCE WITH ME.

YOU WILL FOREVER BE MY ALWAYS, AND I ENJOY DOING LIFE WITH YOU.

TOGETHER IS MY FAVORITE PLACE TO BE AND FOREVER IS THE HOW LONG I WANT TO BE WITH YOU. 

THE REASON I WILL ALWAYS LOVE COMING HOME IS BECAUSE YOU ARE MY HOME. THANK YOU .’

3. Beth Mugo na Nicholas Mugo

Seneta Beth Mugo na mume wake bwana Nicholas Mugo walisherehekea ukumbusho wa miaka 61 katika ndoa.

Beth Mugo ambaye ni binamu yake rais Uhuru kenyatta ni mhusika aliyenusurika kwa ugonjwa wa saratani alisherehekea miaka 80 tangu kuzaliwa kwake.

4. Uhuru Kenyatta na Margaret Kenyatta

Rais Uhuru Kenyatta alifunga ndoa na mke wake Margaret Wanjiru binti yake aliyekuwa maneja wa Kenya Railways bwana Njuguna Gakuo tarehe 2, mwaka wa 1989 katika kanisa la Holy Family Basilica Nairobi.

Kadinali Maurice Otunga ndiye padri aliyewafungisha ndoa.

Wapenzi hawa wamejaliwa watoto watatu Muhoho Kenyatta, Jomo Kenyatta na Ngina Kenyatta.

Kwa sasa, Uhuru na Margaret wanaitwa babu na nyanya baada ya mtoto wao wa kwanza Muhoho na mke wake Achola kubarikiwa na mtoto wao wa kwanza.

Rais Uhuru Kenyatta na mke wake Margaret wameishi katika ndoa kwa miaka 30

5. Raila Odinga na Idah

Aliyekuwa waziri mkuu wa nchi yetu ya kenya bwana Raila Odinga na mke wake Idah wameishi katika ndoa kwa miaka 45.

Katika ukumbusho wao wa ndoa wa miaka 43, Raila aliandika,

‘AS WE CELEBRATE OUR 43RD WEDDING ANNIVERSARY TOGETHER, PEOPLE ASK WHAT THE SECRET TO A LONG, HAPPY MARRIAGE IS.’

kwa sasa ni zaidi ya miaka 40 na wapenzi hawa wanaishi kwa furaha na upendo bado.

6. Miguna Miguna na Jane Miguna 

Jane Miguna ameishi katika ndoa na hakimu Miguna Miguna kwa zaidi ya miaka 17 na pamoja wamebarikiwa watoto 5.

Miguna alikuwa na bibi mwengine lakini walitengana miaka mingi iliyopita.

7. Dorothy Nyong'o na Anyang' Nyong'o

Ingawaje hatujui ni miaka ngapi kamili ambazo gavana huyu wa kisumu ameishi katika ndoa, tuna uhakika kuwa ni zaidi ya miaka 30.

Nyong'o ni baba yake Zawadi Nyongo mwenye umri wa miaka 39, Lupita Nyongo 36, na Peter Nyongo Junior.

7. Ghost Mulee

Mtangazaji wa Radio Jambo bwana Ghost Mulee na mke wake mrembo sana Bi carol wameishi katika ndoa kwa miaka 27.

Kulingana na Ghost Mulee, wawili hawa walikutana kwa matatu zaidi ya miaka 25 iliyopita.

Ghost aliiba roho ya binti Carol kwa kicheko chake cha ajabu sana.

Tangu siku hiyo,wapenzi hawa walianza kuzungmza na mpaka kwa sasa, wanaishi pamoja kwa mapenzi tele.