Matiang’i for PM:Maina Kamanda asema watamwunga mkono Matiangi kuwa waziri mkuu

Matiangi
Matiangi

Mbunge mteule wa chama cha Jubilee Maina Kamanda ameashiria kwamba viongozi wa eneo la kati huenda wakamwunga mkono waziri wa usalama wa ndani kuwa waziri mkuu chini ya mapendekezo yaliyotolewa na  jopokazi la BBI .Kamanda  amemlimbikizia sifa Matiangi akisema  waziri huyo ndiye anayeilinda serikali ya rais Uhuru Kenyatta . Mbunge huyo   aliyasema hayo akiwa Kisii   wakati wa mkutano wa kwanza wa ushauriano kuhusu BBI  uliowaleta  pamoja viongozi kadhaa kutoka sehemu mbali mbali za taifa wakiongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga .Kamanda  aliwahimiza wakaazi wa Kisii Kumlinda  ‘mwanao’ Matiang’I ili wakati mwafaka utakapowadia eneo la mlima Kenya Litamwunga mkono  awe waziri mkuu .

" Hata kazi inayofanywa na mawaziri kutoka kati haiwezi kulinganishwa na kazi anayofanya Matiang'i’ Kamanda alisema huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo . Wakati wa mkutano huo , Raila alisema  jitihada za BBI ndio njia pekee ya kuwafikisha wakenya ‘Canaan’.

Raila amesema taifa litaunganishwa na  BBI  baada ya mwafaka wa ushirikiano kati yake na rais Uhuru Kenyatta  machi mwaka wa 2018 .Raila  amesema kutakuwa na mikutano zaidi ya ushauriano kuhusu BBI  katika sehemu mbali mbali za taifa  kuwaelimisha wakenya kuhusu yaliyomo  katika ripoti hiyo.Matiang'i  aliwasifu Raila na Uhuru kwa  umoja unaoshuhudiwa nchini kwa sasa na kuwahimiza  Viongozi wa Nyanza  kusalia  na umoja ." Hii ndio mara ya kwanza tunaketi pamoja kama viongozi wa Nyanza  ili kujadili kuhusu msimamo mmoja tunaoutaka’ amesema Matiang’I . Matiang’I   amewashauri waakilishi wa kaunti  kuandaa hafla za kuijadili ripoti ya BBI  na wakaazi wa wadi zao .