Matumaini ya familia moja kumpata mwanao yameambulia patupu

Matumaini ya familia moja kumpata mwanao akiwa miongoni mwa manusura wa ajali iliyotokea hivi majuzi huko Kericho imeambulia patupu.

Familia hiyo iliyoko kijijini Gidimo katika kata ndogo ya Galona,Gisambai katika kaunti ndogo ya Hamisi imegubikwa na biwi la simanzi baada ya juhudi zao za kumsaka mwanao kwa siku tatu kugonga mwamba huku mwili wake ukigunduliwa leo katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Russia mjini Kisumu.

Abrahm Madete na Nancy Minayo ni babu na shangaziye kijana huyo na wamekielezea kituo hiki kwamba mwanao alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Chuka na alikuwa akirejea nyumbani kuchukua bidhaa fulani za shughuli za masomo ndipo akapatana na mauti.

Insert-shangazi na babu

Hata hivyo familia hiyo inaomba msaada kutoka kwa serikali na wasamaria wema kuingilia kati na kuwanusuru katika hali hiyo ngumu ikizingatiwa kuwa aila hiyo ni ya pato la chini mno.

Collins Mmbulika