Mauaji City Park: Sikuwa na uhusiano wa kimapenzi na shangazi yangu

bernard chege
bernard chege
Mpwa wa mwanamke aliye pigwa risasi na polisi wawili katika eneo la City park aliambia mahakama ya kwamba hakuwa anafanya mapenzi na shangazi yake alipopigwa risasi na polisi na kuaga.

Janet Waiyaki,41,alipigwa risasi maeneo ya city park alipokuwa na mpwa wake Bernard Chege, 27, aliye pata majeraha katika tukio hilo.

Chege alitoa ushaidi wake jana alipoambia mahakama kuwa amejua uhusiano wake na shangazi ya ke kupitia mtandao.

Aliweza kuulizwa kwanini nguo za shangazi yake za ndani zilikuwa katika gari lake, Chege hakuweza kujibu chochote, mara ya kwanza alisema kuwa hawezi kukumbika chochote, muda baada ya kuulizwa maswali na wakili alisema kuwa nguo hizo hazikuwa za shangazi yake.

Siku moja kabla ya Janet kuuwawa waliweza kusinda pamoja ambapo Janet alimpigia Chege simu aende kwake ndipo Chege aliweza kumuendea nyumbani kwake Donholm na kuelekea Pangani ambapo waliweza kununua Miraa na kuanza kula na marafiki wao wengine.

Aliulizwa walikuwa wanafanya nini usiku wote Chege aliweza kucheza kisha akajibu kuwa "tulikuwa tu wanatafuna miraa."

Kabla ya masaa ya asubuhi kufika Chege waliweza kutoka maeneo hayo na kuelekea maeneo ya Great Rift Valley wakiwa na rafik yao Koome.

Walifika maeneo hayo saa 8:00 asubuhi kwa maana walikuwa wanataka kuona jua likichomoka na kupiga picha kisha kufurahia wakati huo pamoja.

Waliporudi kutoka maeneo hayo Chege aliweza kumuambia Janet ampeleke nyumbani kwake lakini akupuuza kisha akamwambia waende maeneo ya city park.

Alipo fika City Park, Chege alisikia amechoka na kufunga milango ya gari na kutaka kulala alipo kuwa karibu kusinzia aliweza kusikia milio ya risasi kupinduka na kuangalia kwa kioo aliona bunduki katika gari yake ya aina ya (Toyota fielder).

"Niliweza kuingiwa na hofu kisha nikaakisha gari nikaanza kuendesha,lakini kabla ni weze kutoroka eneo hilo lilikuwa limejawa na marisasi,"Alisema Chege

Aliulizwa pia kwanini alikuwa anatoroka  kisha akajibu"Kwa sababu hiyo ndio ilikuwa hatua yangu ya kwanza,"Unahuhakika haukuwa unatoroka kwa sababu ulikuwa unafanya dhabi,"akajibu kuwa "Huo si ukweli."Alijibu Chege.

"Na unaweza sema nini kuhusu nguo za ndani ambazo zilipatikana ndani ya gari yako aliuliza wakili Han Lagat."Zilikuwa za mwanamke,"Nafikiri niza Janet,"Alisema Chege.

Chege alikataa madai kuwa polisi waliweza kumuuliza afungue milango ya gari katika eneo hilo la kitendo hicho bali aliona wanaume watatu

"Baada ya kupigwa risasi niliona nimeumia katika mkono wangu, niliuliza watu waliokaribu kunisaidia ama kupigia ambyulensi simu na hakuna aliyefanya chochote,"Alizungumza Chege.