Mbivu na Mbichi: Gideon na Ruto kukabana koo Rift Valley

gideon and ruto
gideon and ruto
Seneta wa Baringo Gideon Moi jana alikabidiwa rungu ya babake  ili kuashiriwa kukabidhiwa jukumu la  kuiongoza familia yake kisiasa  .

Ilikuwa ni ishara tosha kwamba rais mstaafu  Marehemu Moi  alikuwa amemchagua mwanawe wa mwisho  wa kiume kuchukua usukani wa kuiongoza familia hiyo kisiasa . Watu waliofahamu mipango ya familia Ya Mzee  Moi wamesema kabla hata ya  hafla ya jana ya Gideon kukabidhiwa rungu hiyo na kakake Raymond ,Moi alikuwa ameshatangaza kabla ya kifo chake kwa Gideon Ndiye atakayemrithi kisiasa.

Kingpin? Gideon Moi apewa ‘rungu’ ya Mzee Moi na familia yake.

Kisha alianza kumfunza mambo ya kumwezesha kuchukua jukumu hilo na tangia hapo Gideon Moi alikuwa karibu sana na babake . Inafahamika kwamba Mzee Moi ndiye aliyemshinikiza mwanawe kujiunga na siasa  na pia kukiongoa chama Cha KANU .

Kuidhinishwa kwa Gideon kama mrithi wa Mzee Moi sasa huenda kukafungua wamu nyingine kali ya  malumabno ya uongozi wa jamii ya wakalenjin na naibu wa rais William Ruto . Gideon  hakutarajiwa kulingana na mila za wakalenjin kuwaruka kakake zake wakubwa marehemu Jonathan na mtoto wa pili wa Mi Raymond ili kuchukua usukani wa kisiasa wa familia yake . Lakini uamuzi wa familia kubwa ya Chepkeres  kumpa uongozi wa kisiasa wa familia huenda  umethibitisha uamuzi wa marehemu Mzee Moi . Baada ya Gideon kupewa jukumu hilo ,hofu iliyokuwepo  ya uwezekano wa kuzuka mgawanyiko sasa imefutiliwa mbali .