Mahakama ya Kiambu siku ya jana iliyaskiza mashataka ya vile ambavyo mwanasiasa wa zamani alihusika na kifo cha mke wake wa hapo awali.
Ripoti ya postmortem ilionyesha kuwa, Lucy Njambi, alinajisiwa, akalazimishwa kunywa asidi na kuchomwa nayo.
Mca wa hapo awali Samwel Ndungu, anakabiliwa na mashtaka ya kumuua Lucy mwezi wa Januari.
Sergeant Linus Mugambu aliiambia mahakama kuwa aliweza kuongea na mwathirika katika hospitali ya kata kabla yake kuiaga dunia kutokana na majeruhi aliyoyapata.
Lucy alimsimulia vile ambavyo alitekwa nyara akiwa kwa gari ya bwanake kabla ya kupelekwa kwenye shamba la kahawa.
Afisa yule aliiambia mahakama kuwa dakika chache kabla ya Lucy kuiaga dunia, mwathiriwa yule alimwambia yeye na jamaa zake kuwa ilikuwa ni bwana yake aliyepanga mpango wa kumshambulia.
Lucy alisema kuwa Samuel alienda kumtembelea kule Ruiru na walipokuwa wanaongea, wanaume wawili na mwanamke mmoja waliingia kwa gari na kuanza safari ambapo walisimama kwenye shamba la kahawa ambapo Lucy alibakwa na kulazimishwa kunywa asidi.
Samuwel Ndungu anashtakwia pamoja na Joyce Njambi na Wilson Mwangi katika kesi ile ya kutekeleza mauaji.
Kesi hiyo yaendelea leo.
Soma mengi