Madaktari na wauguzi katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Kaunti ya Kakamega walitoroka kutoka wadi moja baada ya mgonjwa aliyekuwa na daalili kama za virusi vya Corona kuletwa .
Wahudumu hao wa afya walihofia kuambukizwa ugonjwa huo kwa sababu hakuwa na vifaa vya kutosha kujikinga .
Tukio hilo lilizua hofu katika hospitali hiyo na baadaye mwendo wa saa sita mchana msimamizi wa hospitali hiyo alipoagiza kufungwa kwa Milango yote ya kuingia kwenye taasisi akisema hakuna mgonjwa mwingine atakayeruhisiwa kuletwa . Mgonjwa huyo baadaye alipelekwa katika wadi iliyotengwa ndani ya hospitali .