'Miaka 13 baadae mungu amenipa malkia mwingine!' Kate atangaza

KATE (1)
KATE (1)
Kwa mda sasa, wakenya kwenye mtandao wa kijamii wamekuwa wakidokeza kuwa muigizaji Kate almaarufu, Kate Actress ni mja mzito.

Hata hivyo Kate alijittetea kila mara akisema kuwa tumbo lake lilikuwa limefura, na wengi wakamuamini huku wakidhani ni umbea tu.

Hata hivyo, miezi kadhaa baadaye aliamua kutangaza habari njema huku akifichua kuwa anatarajia mwana mwingine.

Miaka 13 baadaye, mrembo huyu aliamua kujaribu uzazi tena. Kate alijaliwa mwana wake wa kwanza akiwa msichana mdogo kimiaka na anafichua kuwa hakujua jinsi jambo hilo lingemuadhiri. Hata hivyo, ana furaha zaidi kuwa mumewe Phil alivumilia naye ikijulikana kuwa mashabiki wao walikuwa wanawaskuma zaidi kupata mtoto pamoja.

Aliandika,

@phil_director Thank you for your patience, I had no idea how much being a teenage mum affected me. You gave me assurance that you would never leave us, you have held my hand all through, spoilt me silly, I am indeed blessed. We thank God, This is such an honor 🙏🏿❤️

Kate hata hivyo, hakufichua jinsia ya mwanao kwani alimuita tu 'K'.

The cat or rather the baby is out of the bag 😊! We are over the moon, We really wanted to keep this to ourselves but then again I remembered the many women on my timeline, hopeful moms to be, rainbow mums, career women trying to decide between family and your goals. I feel you, this is for you, Gods time is the best! @phil_director hey daddy ❤️

#BabyK

Muigizaji huyu ana unyenyekevu mkuu kuwa mama kwa mara nyingine tena na amebarikiwa kuwa na mume ambaye humshika mkono kila mara.

I have always been the Helicopter Mom, 13 years later, God has given me another opportunity to raise another angel, I am humbled. I feel blessed, I don’t know how this experience is going to be, but am willing to let go, am no longer the paranoid mom. We are protected 😘🙏🏿❤️

Catherine Kamau/ Instagram

Kutoka kila mmoja hapa Radio Jambo, tunawapa wapendwa hawa wawili hongera huku tukiwatakia mema, maishani mwao.

Zifuatazo ni picha walizopiga huku wakikaribia kumkaribisha mwanao: