•Omanyala aliishindia Kenya dhahabu ya kwanza kabisa katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola.
•Omanyala amesherehekea ushindi wake na kuwashukuru wote waliounga mkono azma yake ya kutwaa ubingwa.
Ferdinand Omanyala sasa sio tu bingwa wa Kenya na Afrika bali pia ni bingwa wa Jumuiya ya Madola mwaka wa 2022.
Jumatano usiku mwanaspoti huyo mahiri aliishindia Kenya dhahabu ya kwanza kabisa katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola.
Omanyala alimaliza wa kwanza katika mashindano yanayoendelea jijini Birmingham, Uingereza baada ya kukimbia kwa sekunde 10.02.
Akani Simbine wa Afrika Kusini alimaliza nyuma ya Omanyala kwa sekunde 10.13 huku Yupun Abeykoon wa Sri Lanka akichukua nafasi ya tatu baada ya kukimbia kwa sekunde 10.14.
Pengo kubwa (sekunde 0.11) kati ya bingwa huyo anayeshikilia rekodi ya Afrika katika mbio za mita 100 na aliyeibuka wa pili linaonyesha wazi kuwa aling'aa zaidi mno ya wapinzani wake.
Omanyala amesherehekea ushindi wake na kuwashukuru wote waliounga mkono azma yake ya kutwaa ubingwa.
Isaya 55.5 , Kwa utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. Asanteni sana kwa uungwaji mkono na motisha," Omanyala alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter.
Aliongeza "BINGWA WA AFRIKA sasa ndiye BINGWA WA JUMUIYA YA MADOLA!"
Wakenya wengi wameendelea kumpongeza bingwa huyo wa mbio za mita 100 kupitia mitandao ya kijamii.
Omanyala takes the gold!!! @Ferdiomanyala
— Maina Kageni (@ItsMainaKageni) August 3, 2022
Africa’s fastest man, a son of our soil, @Ferdiomanyala, you have made our entire nation proud.
— Raila Odinga (@RailaOdinga) August 4, 2022
Your victory exemplifies the results of focus, courage, consistency, and sacrifice.
Congratulations! pic.twitter.com/Zls4IRgoZJ
Gold is here! @Ferdiomanyala wins #Birmingham2022 #birminghamcommonwealthgames2022 100 metres men Gold. pic.twitter.com/HesmG4v4g7
— Manoah Esipisu MBS (@MEsipisu) August 3, 2022
Ushindi huu wake unajiri wiki chache tu baada ya kuandikisha matokeo ya kukatosha tamaa huko Oregon, Marekani.
Mwezi jana Omanyala alibanduliwa nje ya mashindano ya dunia katika hatua ya nusu fainali baada ya kumaliza wa tano katika kundi alilowekwa.
Kucheleweshwa kwa safari yake kuenda Marekani kulinyooshewa kidole cha lawama kufuatia matokeo hayo kwani ni wazi kuwa hakupata muda tosha wa kujiandaa.
Hata hivyo mwanaspoti huyo sasa ana sababu za kutabasamu kwani hatimaye ameweza kung'aa katika jukwa la kimataifa
Hongera bingwa wetu Ferdinand Omanyala!