Gudaf Tsegay alipiga magoti mbele yangu na kuniomba msamaha – Faith Kipyegon

Kipyegon alisema kwamba alimsamehe Tsegay kwani huu ni mchezo na kaitka mashindano yoyote, wanamichezo huhitajiana kwani mmoja hawezi kushindana peke yake.

Muhtasari

Hata hivyo, alivuliwa nishani hiyo kutokana na kuzozana na Gudaf wa Ethiopia wakati wa mbio hizo ambazo alishinda mwanamfalme Beatrice Chebet.

FAITH KIPYWGON AKIRI KUMSAMEHE TSEGAY
FAITH KIPYWGON AKIRI KUMSAMEHE TSEGAY
Image: FACEBOOK

Mwanariadha Faith Kipyegon amefunguka kuhusu mpambano wake mkali na Gudaf Tsegay wa Ethiopia kwenye Mashindano ya Olimpiki ya Paris 2024.

Kipyegon amefichua kuwa amemsamehe mwenzake baada ya kuomba msamaha kwa ugomvi uliosababisha Mkenya huyo kupokonywa fedha yake na kurejeshewa baada ya muda wakati wa mbio zao za mita 1500m

Kipyegon aliondoka huku akilia baada ya kufikiria kuwa alitwaa medali ya fedha kabla ya kunyakua medali ya dhahabu kutoka mbio za 1500m mjini Paris 2024.

Hata hivyo, alivuliwa nishani hiyo kutokana na kuzozana na Gudaf wa Ethiopia wakati wa mbio hizo ambazo alishinda mwanamfalme Beatrice Chebet.

Kipyegon sasa amejitokeza kueleza kuwa Tsegay aliomba msamaha baada ya kisa hicho na hakupoteza muda kujisalimisha.

"Alikuja baada ya heat za mita 1500, akapiga magoti mbele yangu na kuniomba nimsamehe," alisema kulingana na Nation Africa.

faith kipyegon,
faith kipyegon,

“Nilimsamehe kwa sababu huu ni mchezo na ninamuhitaji kwenye mashindano. Tunahitajiana kila mmoja kujiweka kikomo na kuvunja rekodi."

Akisimulia kilichotokea, mwanariadha huyo mwenye kipaji alibainisha kuwa alijaribu sana kukwepa kuingia kwenye mstari kwani ingemsababishia kutofuzu moja kwa moja.