EURO 2020

Hatimaye EURO 2020 kuanza Ijumaa usiku

Tazama makundi yalivyopangwa, Kundi F ndilo la kuangaziwa zaidi

Muhtasari

•Michuano hiyo ilifaa kuchezwa mwaka jana ila ikaahirishwa hadi mwaka huu kutokana na mlipuko wa homa ya COVID 19  

•Kundi la kuangaziwa sana ni kundi la F ambalo lina wachezaji matata wakiwemo Christiano Ronaldo, Kieran Mbappe, Manuel Nuer na wengine

Mataifa 24 yatashirikishwa kwenye michuano ya EURO 2020
Mataifa 24 yatashirikishwa kwenye michuano ya EURO 2020
Image: Hisani

Hatimaye michuano ya EURO 2020 iliyokuwa imesubiriwa sana inatarajiwa kuanza usiku wa Ijumaa, Juni 11.

Michuano hiyo ambayo ilifaa kuchezwa mwaka jana ila ikaahirishwa hadi mwaka huu kutokana na mlipuko wa homa ya COVID 19  unatarajiwa kuanza na mechi kati ya Uturuki na Italia itakayochezwa saa nne usiku, masaa ya Afrika Mashariki.

Jumla ya mataifa 24 ya Bara Ulaya yameshirikishwa kwenye Kombe hilo linalotarajiwa kuchezwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Mataifa yanayoangaziwa sana ni pamoja na mabingwa wa kombe hilo mwaka wa 2016 Ureno, Uingereza, mabingwa wa Kombe la dunia Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ubelgiji na Uhispania.

Michuano hiyo imegawanyishwa katika makundi sita yenye timu nne kila kikundi. Haya hapa makundi hayo;

Kundi A:Uturuki, Uswisi, Italia, Welisi

Kundi B: Urusi, Ubelgiji, Udenmarki, Ufini

Kundi C: Austria, Uholanzi, Masedonia Kaskazini, Ukreni

Kundi D: Ucheki, Kroatia, Uskoti,, Uingereza

Kundi E: Uswidi, Poland, Uhispania, Slovakia

Kundi F: Ujerumani, Ufaransa, Ureno, Hungaria

Kundi la kuangaziwa sana ni kundi la F ambalo lina wachezaji matata wakiwemo Christiano Ronaldo, Kieran Mbappe, Manuel Nuer na wengine