Mflame wa Asisti: Kevin De Bruyne atoa asisti katika utunzi wa wimbo wa Drake

Wick Man, wimbo wa 27 kwenye albamu mpya ya Drake 'For All The Dogs - Scary Hours Edition' ina watunzi watatu waliotajwa katika utayarishaji wa wimbo huo, jina la De Bruyne likionekana.

Muhtasari

• Wick Man, wimbo wa 27 kwenye albamu mpya ya Drake 'For All The Dogs - Scary Hours Edition' ina watunzi watatu waliotajwa katika utayarishaji wa wimbo huo.

• Wao ni A.Graham (Drake), A.Mamam (Mtayarishaji wa New York anayejulikana kama The Alchemist) na K. De Bruyne.

Kevin De Bruyne na Drake
Kevin De Bruyne na Drake
Image: Insta

Kiungo huyo wa kati wa Manchester City anaonekana kutumia muda wake nje ya uwanja kwa matumizi mazuri wakati bado anauguza jeraha lililomweka nje kwa miezi kadhaa.

Mashabiki wa rapa wa Kanada, Drake walishtuka baada ya kugundua kuwa Kevin De Bruyne anaonekana kutajwa kuwa mmoja wa waliotoa mchango katika kuandika tungo ya wimbo wa msanii huyo.

Wick Man, wimbo wa 27 kwenye albamu mpya ya Drake 'For All The Dogs - Scary Hours Edition' ina watunzi watatu waliotajwa katika utayarishaji wa wimbo huo.

Wao ni A.Graham (Drake), A.Mamam (Mtayarishaji wa New York anayejulikana kama The Alchemist) na K. De Bruyne.

Ingawa bado haijathibitishwa kama huyu ni Kevin De Bruyne wa Manchester City, amepewa sifa kama mwandishi kulingana na tovuti ya muziki ya Genius.

De Bruyne ameondolewa kwenye mchezo wa soka tangu mwezi Agosti kutokana na jeraha la misuli ya paja lililohitaji kufanyiwa upasuaji.

Lakini inaonekana kana kwamba amekuwa akitumia muda wake nje ya uwanja kwa matumizi mazuri kwa kuingia studio pamoja na Drake.

Wimbo wenyewe hauna marejeleo ya soka ndani yake na zaidi unazingatia maisha ya Drake na beef za kurap.

Katika wimbo huo, Drake anaonekana kufungua tena ugomvi wa muda mrefu na rapa mwenzake wa Marekani Pusha T.

Mashabiki kwenye X, ambayo zamani ilijulikana kama Twitter walikuwa wepesi kutania kuhusu mchango wa De Bruyne nje ya uwanja.

Akaunti moja iliandika: "Hata wakati hachezi bado anatafuta njia ya kusaidia mtu kwa kutoa asisti."

Shabiki mwingine aliandika: "Msaidizi mzuri kutoka kwa KDB lakini wakati huu kwa DRAKE."

Wa tatu aliandika: "Amezaliwa kusaidia."

Manchester City wanatumai kuwa De Bruyne anaweza kurejea katika utimamu wake kabla ya mwaka mpya huku Pep Guardiola akitoa taarifa kuhusu utimamu wake wiki hii.