Haaland avunja kimya kuhusu meme yake akimfokea refa kwenye mechi dhidi ya Spurs

Picha moja ilionyesha Haaland katika kipengele chake cha hasira, lakini ilipigwa picha kwenye kipande cha mchoro.

Muhtasari

• Picha moja ilionyesha Haaland katika kipengele chake cha hasira, lakini ilipigwa picha kwenye kipande cha mchoro.

Erling Haaland
Erling Haaland
Image: X

Fowadi wa Manchester City, Erling Haaland amevunja kimya chake kuhusu picha yake akimfokea refa wakati wa mechi yao dhidi ya Tottenham Hotspurs wikendi.

Picha hiyo imegeuzwa meme na wengi wamekuwa wakiieneza kwa jinsi ambavyo raia huyo wa Norway alikuwa amafoka kwa hasira dhidi ya muamuzi wa mechi hiyo iliyoishia sare ya mabao 3-3.

Mambo yangeenda tofauti kama mwamuzi Simon Hooper alicheza kwa faida katika dakika za kufa wakati Grealish alifunga bao.

Hooper alipuliza kipenga cha kumfanyia madhambi Haaland, na kumaliza shambulizi hilo na kumwacha mshambuliaji na wachezaji wengine wa Manchester City wakiwa wamekasirishwa na uamuzi huo.

Halaand aliadhibiwa kwa maandamano yake, lakini huo haukuwa mwisho kwani aliendelea kumzomea mwamuzi baada ya kipyenga cha muda wote.

Kama ilivyoripotiwa na BBC, Haaland baadaye alishiriki hisia zake kwenye mitandao ya kijamii, akichapisha picha za tukio hilo pamoja na maelezo mafupi.

Uamuzi wa utata wa Simon Hooper unaweza kuwa ndio mazungumzo ya kwanza baada ya mchezo. Hata hivyo, hiyo ilibadilika Jumatatu, Desemba 4 huku watumiaji wa mtandaoni wajanja walipoona upande wa kuchekesha wa kejeli za Haaland, Sports Brief walibaini.

Meme ya Haaland tangu wakati huo yamekuwa yakisumbua mitandao ya kijamii, na mshambulizi huyo wa zamani wa Borussia Dortmund alifurahishwa na baadhi ya picha za ubunifu zinazosambazwa mtandaoni.

Picha moja ilionyesha Haaland katika kipengele chake cha hasira, lakini ilipigwa picha kwenye kipande cha mchoro.

Alisema kwamba meme hiyo kwa mara ya kwanza ilimfanya kutabasamu mwenyewe.