Korti yazidisha muda wa kuzuia wabunge kulipwa marupurupu ya nyumba
WABUNGE wamepata pigo baada ya mahakama kuzidisha muda wa agizo la kuwazuia kupokea marupurupu ya nyumba ya shilimngi elfu 250 kila mwezi . SRC ilikuwa imewasilisha kesi ikitaka wabunge kuzirejesha fedha hizo walizokuwa wamelipwa ikisema hatua hiyo ni ukiukaji wa sheria . agizo hilo litaendelea kutekelezwa hadi juni tarehe 24 wakati kesi hiyo itakaposikizwa .
Mtoto aliyeibwa Naivasha afariki
Mtoto mchanga anayeshukiwa kuibwa na mwanammke mmoja huko naivasha ameaga dunia baada ya kupata matatizo ya kupumua . naibu OCPD wa naivasha JoHN Kwasa AMESEMA mwanamke aliyekuwa amemwiba mtoto huyo anahojiwa na polisi .
Maafisa 10 wa KDF katika ajali ya barabarani .
Maafisa kumi wa KDF wanapokea matibabu katika hospitali ya Forces memorial baada ya kujeruhiwa katika ajali ya barabarani katika eneo la mutindwa kwenye barabara ya kangundo mapema leo . kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya matungulu ISAAC thuranira amesema dreva wa lori hilo lililokuwa limewabeba maafisa 18 wa KDF alishindwa kulithibiti na kulifanya kulisababisha kuanguka
Mvua kutawala Kisumu,Siaya na Homabay
Kaunti za Kisumu, Siaya, Homabay, Kericho na Nakuru c ni baadhi ya zinazotarajiwa kushuhudia mvua kubwa katika siku tano zijazo . idara ya utabiri wa hali ya anga imesema hali ya kibaridi na mawingu itatawala sehemu za Nairobi, Nyandarua, Laikipia, Nyeri, Meru, Embu na Tharaka Nithi .
Wachina wanaofanya biashara ndogo ndogo kurejeshwa nchini mwao-Matiang'i
Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiangi ameaigiza kurejeshwa nchini mwao raia wa Uchina wanaofanya biashara katika soko la Gikomba hapa jijini . Matiangi amesema wachina hao wapo nchini kinyume cha sheria . Matiangi amesema raia wote wa kigeni wanaoshiriki biashara ndogo ndogo nchini watarejeshwa makwao.
Mtoto aliyeambukizwa ebola Uganda afariki
Mtoto mwenye umri wa miaka mitano nchini Uganda aliyepatikana na virusi vya Ebola ameaga dunia .shirika la afya duniani WHO limesema kisa hicho kilikuwa cha kwanza kilichothibitishwa nchini humo baada ya kuchipuka kwa ugonjwa huo katika taifa la DRC .
Mwalimu auawa ,Polisi 2 wajeruhiwa katika shambulzi la majangili Turkana
Mwalimu mmoja wa shule ya msingi ameuawa kwa kupigwa risasi ilhali maafisa wawili wa polisi wa utawala wamejeruhiwa baada ya gari la polisi kushambuliwa na majangili huko Turkana mashariki .kamanda wa polisi wa kautni ya Turkana Samuel Ndanyi amesema gari hilo la polisi lilikuwa likielekea katika kituo cha kibiashara cha Lokori kutoka Napeiton .
Mwanamme amwua mkewe Matayos
Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 25 ametorokea mafichoni baada ya kumuua mkewe kwa kumudunga kisu katika eneo la Khujibi , Matayos kaunti ya Busia. Jamaa huyo anadaiwa kuanza kumpiga mkewe wakati wa usiku kabla ya majirani kuingilia kati ingawa mkewe alifariki baadaye kutokana na majeraha ya visu.
Nakuru sasa ni kituo cha huduma za paspoti
Iwapo unaishi nakuru au maeneo yanayopakana na mji huo basi una cha kukupa tabamasamu kwani hutalazimika kupiga kambi katika jumba la nyayo hapa Nairobi kupata paspoti au kubadilisha iliyojaa . waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi amesema tangu septemba mwaka wa 2017 takriban watu milioni moja wamepata paspoti mpya au kuchukua za kisasa .
FBI kuisadia Kenya kupambana na ufisadi
Shirika la uchunguzi nchini marekani FBI liemeahidi kuisaidia Kenya katika vita dhidi ya ufisadi .hii ni baada ya mkutano kati ya mkuu wa dci George kinoti ,mkurugenzi mkuu w amashaka ya umma Noordin Haji na naibu mkurugenzi wa FBI David Bowdich . kundi hilo lipo katika ziara ya siku tatu nchini marekani .
City hall yatangaza wazi nafasi za maafisa wakuu
City Hall imetangaza wazi nafasi kumi za wakuu wa idara ,mkurugenzi wa zabuni na katibu wa jiji .hii ni baada ya ufichuzi kwamba kandarasi za baadhi ya maafisa wakuu wa CITY hall zilitamatika mwezi aprili .una hadi tarehe 24 kutuma maombi ya kazi hizo .
Bunge la Murang’a lapitisha bajeti yake ya 2019/2020
Bunge la kaunti ya murang’a limeidhinisha bajeti ya shilingi bilioni 8.9 ya mwaka wa 2019/2020. Mwenyekiti wa kamati ya bajeti Kibe Wasare amesema baadhi ya idara zilizonufaika pakubwa na bajeti hiyo ni afya ,kilimo ,kawi ,elimu na miundo msingi .