Mkusanyiko wa Habari zote Muhimu Leo Jumatatu 14/10/2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC

Mgane wa  marehemu gavana wa Bomet Joyce Laboso,  ameteuliwa kuwa  mwanachama wa kamati ya ushauri kuhusu mashirika ya serikali .katika  uteuzi uliotangazwa  na rais Uhuru kenyatta kupitia arifa maalum ya gazeti rasmi la serikali  Edwin Abonyo  atakuwa mwanachama wa kamati hiyo kwa miaka mitatu ijayo. Abonyo ni miongoni mwa watu saba walioteuliwa .kwingineko waziri wa leba Ukur Yattani amemteua mbunge wa zamani wa Othaya Mary Wambui kuwa mwenye kiti  maamlaka ya  kitaifa ya ajira  kwa kipindi cha miaka mitatu .

Wenye magari watapata afueni mwezi huu baada ya mafuta ya petroli na diesel kupungua kwa mujibu wa tathmini mpya iliyotangazwa na tume ya Petroli na kawi . lita moja ya  petrol hapa jijini itauzwa kwa shilingi 108 Nukta 05 kutoka shilingi  112 na senti 81 .lita moja ya disel itauzwa kwa shilingi 101 na senti 96 kutoka bei ya awali ya shilingi 103 nukta 03 . bei ya mafuta taa hata hivyo imepanda hadi shiingi 101 nukta 08 kutoka shilingi 100 na senti 64 .

Bunge la  Kaunti ya Busia ndilo la hivi punde kuukata mswada wa punguza mizigo uliopendekezwa na chama cha Thirdway Alliance .waakilishi wa kaunti wamesema wananchi hawakuhusishwa katika kutayarisha mswada huo na vile vile utarejesha nyuma hatua zilizoafikiwa kufanikisha ugatuzi .

Chuo kikuu cha Moi Kimewafurusha  viongozi watano wa wanafunzi  ambao wanadaiwa kupanga maandamano yaliokumbwa na ghasia wiki jana  na kusababisha chuo hicho kufungwa kwa muda usiojulikana .  naibu chansella Isaac Kosgey  amethibitisha kwamba wanafunzi hawatakubaliwa kurejea shuleni humo .

Mahakama moja mjini Voi imempata na hatia mwanamume mwenye umri wa miaka 56  aliyembaka  bintiye mwenye umri wa miaka 17.Mwemba Gereza anadaiwa kutekeleza kitendo hicho Agosti 28 mwaka 2016 katika eneo la Buguta huko Voi.Hakimu mkaazi wa Voi Fredric Nyakundi amesema upande wa mashtaka ulidhibitisha kuwa mshukiwa alitekeleza kitendo hicho cha kinyama

Familia za wakenya waliofariki katika ajali ya ndege ya  Ethiopia hatimaye zimekubaliwa kuichukua miili ya wapendwa wao . waziri wa mashauri ya  kigeni Monica Juma amesema miili yote  imetambuliwa huku 28 ikiwasili  nchini kwa maazishi ilhali iliosalia itachomwa.miili mingine ya waliokuwa na uraia wa zaidi ya nchi moja  itazikwa kwa mujibu wa matakwa ya familia .

Wazazi wameshauriwa kukoma kuwapa shinikizo wanafunzi kufanya vyema katika mitihani ya kitaifa .waziri wa elimu George Magoha  pia amewataka watahiniwa wa mwaka huu kutoitikia kuwekwa chini ya shinikizo kwani kila mmoja atasonga katika hatua ifuatayo ya elimu bila kujali matokeo yake .

  TSC imewapiga marufukua walimu waliohusika na visa vya udanganyifu  katika mitihani ya hapo awali dhidi ya kusimamia mitihani ijayo ya KCPE na  KCSE . Afisa mkuu wa  tume hiyo  Nancy Macharia  amesema katika miaka mitatu iliyopita ,wamewachukulia hatua walimu 144 waliohusika na udanganyifu katika mitihani ya kitaifa .

Kiongozi wa walio wengi katika bunge  la kaunti ya  Nairobi Abdi Guyo  ameandikisha taarifa na DCI akidai kamba maisha yake yamo hatarini . Amesema kizazaa kilichotokea city hall wiki jana kilipangwa na magenge yalitumwa katika bunge la kaunti kusambaratisha shughuli .

Mshikilizi wa rekodi ya dunia katika mbio za marathon Eliud Kipchoge  ametaka kukutana na rais wa zamani wa marekani Barrack Obama .hii ni baada ya Obama kumtumia ujumbe wa kumhongera katika twitter  kwa kumudu kumaliza mbio za marathon chini ya saa mbili .Obama pia alimtambua  Brigid Kosgei kwa kuvunja rekodi ya akina dada katika mbio za marathon..Kipchoge anataka kukutana na Obama ili kujadili jinsi ya kuufanya ulimwengu kuwa bora zaidi .

SERIKALI imeshtakiwa kwa kuondoa  paspoti za kidiplomasia za  majaji wa mahakama kuu  na kuwazuia kutumia maeneo ya watu mashuhuri katika viwanja vya ndege .  mkenya ,jonathan Munene  amesema hatua hiyo inatishia uhuru wa idara ya mahakama  na nataka arifa hiyo ya kisheria kufutiliwa mbali .

Waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi  amefutilia mbali likizo ya maafisa wakuu wa polisi  ili waweze kuangazia kikamilifu mitihani ijayo ya kitaifa . matiangi pia amewahakikishia wakenya kwamba hapatakuwa na  udhaifu wa kiusalama wakatai wa mitihani hiyo.

Watoto wa Kenya ni werevu na hawahitaji  kushiriki udanganyofu ili kupita mtihani .waziri wa elimu George magoha  amewatahadharisha walimu ,wazazi  na maafisa wa elimu ambao huenda wana njama  ya kujaribu kuwasadia wanafunzi kufanya udanganyifu katika mitihani ya kitaifa .

Usijaribu kuyatumia maneno ya kujifanya ni kama unafahamu wanayopitia watu wenye  maradhi kama vile kansa au kuwamabia kwamba kila jambo hutendeka kwa ajili ya sababu Fulani . mwanasaikolojia  Riziki Ahmed  amesema matamshi kama hayo huwavunja moyo wagonjwa  hao.

Video ya dakika 47  iliyorekodiwa   ya Peter Ngugi aliyekuwa akiwapasha polisi habari  akikiri kuhusika na mauaji ya wakili Willie Kimani  haitachezwa kortini .jaji  amesema  afisa aliyerekodi video hiyo  hakufutwa kanuni zifaazo wakati wa kuichukua video hiyo iliyofaa kutumiwa kama ushahidi .

Miili ya  wakenya walioaga dunia  katika ajali ya ndege  ya  shirika la Ethiopia  airlines imewasili katika uwanja wa ndege wa JKIA  ili kuchukuliwa  na jamaa zao .miili 28 kati ya 32 ya wakenya  hao walioafriki katika mkasa huo imewasili mapema  leo katika uwanja huo  .watu 157 waliangamia katika ajali hiyo mwezi machi .

 

Uhaba wa walimu huko taita taveta unachangia kudorora kwa ubora wa elimu  .mbunge wa mwatate  Andrew Mwadime  aniataka tume ya kuwajiri walimu TSC  kuwaajiri walimu zaidi  katika eneo hilo kwani kuna vijana wengi waliohitimu kuwa walimu lakini hawana kazi .

Mbunge wa kitui  mashariki Nimrod Mbai  anataka kamishna wa kaunti ya Kitui John Ondego ahamishwe kwa  madai ya kukosa kurejesha hali ya usalama katika eneo hilo  linaloshambuliwa mara kwa mara na wafugaji wa ngamia . Mbai amesema wenyeji sasa wamelazimika kuishi katika kambi za muda  ilhali serikali haijachukua hatua zozote madhubuti za kuwalinda .Odengo hata hivyo amekana kuwyatelekeza maslahi ya wakaazi hao.

Chama cha ODM kimetakiwa kuwahakikishia wakenya kwamba kitadumisha amani wakati wa uchaguzi mdogo wa kibra .mbunge wa  kiharu Ndindi Nyoro  amesema kisa kama  kilichotokea mwishoni mwa wiki ambapo msafara wa mgombeaji wa Jubilee Mcdonald mariga ulishambuliwa kwa mawe  sio jambo linalofaa kukubaliwa .

Serikali itazidisha mara dufu jitihada za kukabiliana na udanganyifu katika mitihani ya kitaifa mwaka huu .afisa mkuu mtendaji wa  baraza la kitaifa la mihani Mercy Karogo  amewashauri  maafisa wakuu wa elimu katika kaunti ndogo kuhakikisha kwamba  wanafuatilia kikamilifu   usimamizi   wa zoezi la mtihani katika maeneo yao .

Wakaazi wa Mombasa wanaitaka serikali kuboresha usalama katika feri  ili kuzuia maafa siku za usoni . wamesema baadhi ya  sehemu za feri zinafaa kuboreshwa na pia kuweka vifaa vya kuwawezesha watu kujiokoa wakati panapotokea  dharura .