Polisi wanalisaka genge la majambazi waliomwua mlinzi mmoja huko Ukunda, Kwale kwa kumkatakata na kisha kuiba kompyuta mbili katika afisi aliokuwa akilinda.
Kamishna wa kaunti ya Kwale Kutswa Olaka amesema wanachunguza mauaji hayo na iwapo yanayahusiana na vita dhidi ya washukiwa wa biashara ya dawa za kulevya.