'Mpenzi wangu wa maisha,'Diamond asherehekea siku ya kuzaliwa ya mwanawe

Staa wa nyimbo za bongo Diamond Platnumz na mwana sosholaiti Hamissa Mobetto hii leo wameandika jumbe za mahabara kwa mwana wao Dylan ambaye amefikisha miaka mitatu hii leo.

Wawili hao walikuwa wapenzi lakini watengana kwa sababu moja au nyingine huku wakiwa wamebarikiwa na mtoto mmoja, wawili hao wanasaidiana kumlea mtoto wao kwa vyovyote vile.

Kupitia kwenye mitandao ya kijamii Diamond aliandika ujumbe huu kwa Dylan;

"Happy birthday kwa mpenzi wangu mwingine wa maisha @DEEDAYLAN ❤🌹❤." Aliandika Diamond.

Kwa upande mwingine Hamisa naye aliandika ujumbe wa kusherehekea siku za kuzaliwa za mtoto wake na huu hapa ujumbe wake;

"Mwanangu ambaye amebarikiwa mwenye neema na hata mwenye urembo kupindukia amefikisha miaka mitatu hii leo, muda umeenda kwa kasi siku hii ya leo nakutakia kila la heri na uwe jinsi Mungu alikuwa amekupangia kuwa katika maisha yako

Uzuri na neema iwe nawe kila mara na zisiweze kukuacha maishani mwako asante sana kwa kunichagua niwe mama yako HAPPY 3RD BIRTHDAY SON. @DEEDAYLAN 👑nakupenda sana." Aliandika Hamisa.

Kutoka kwetu wanajambo tunamtakia siku njema, huku akisherehekea siku hii yake ya kipekee.