Mudavadi amesema wakenya wanafaa kukumbuka kwamba maelfu ya wakenya walipoteza maisha yao kwa sababu ya siasa kama hizo . Amesema alikuwa miongoni mwa viongozi waliohusika na mazungumzo ya kuleta Amani nchini wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka wa 2007.
Mudavadi amesema ni ukosefu wa uajibikaji kwa viongozi kutumia matusi ili kuzua mgagawanyiko wa kikabila .
" Tuheshimu maoni ya kila mmoja . hakuna aliye na haki ya kumtukana mwenzake . Mbona mtu amlenge mama Ngina kisiasa?’ Musalia alihoji kuhusu matamshi aliotoa mbunge wa Oscar Sudi na mwenzake Johana Ng’eno .
Mudavadi amesema Umoja wa sio jambo linalofaa kuibngizwa mzaha kwani ustawi wa taifa unategemea umoja wake .
Mudavadi aliyazungumza hayo katika shule ya msingi ya Gaitheri huko kiharu wakati wa mazishi ya mwakilishi wa wadi ya Gaturi Kiiru Mwangi kwa jina maarufu Mbembe aliyeaga dunia wiki jana .