Muigizaji Celina Njoki awekwa ICU Kijabe

101682016_164016748461051_3081798247056764730_n
101682016_164016748461051_3081798247056764730_n
Muigizaji na mwanahabari wa kituo cha Gheto Radio Celina Njoki anaripotiwa kuwa mgonjwa na kulazwa katika hospitali ya Kijabe siku chache tu baada ya kubarikiwa na mtoto mvulana.

Kulingana na rafikiye wa karibu Veronica Mwaura ambaye ameandika katika ukurasa wake wa Facebook, amesema Njoki anahitaji damu ya O+ ama O- na kuwasihi wakenya walio na damu aina hiyo kujiwasilisha katika Hospitali kuu ya Kijabe ili kumsaidia.

"I need your help my friend, actress, and radio presenter, Celina Njoki, urgently needs blood. Blood group 0+ or 0-. I'll appreciate it, ready to send uber or fare to Westlands. As well as pick you. Browngirl needs us now,"ameandika Mwaura.

Veronica amesema kuwa Njoki amewekwa kwa mashine ya ICU japo ameonyesha dalili kubwa ya kupona .

Amepeana maeneo toafauti ambayo mkenya yeyote ambaye anaweza kujiwasilisha ili kutoa mchango wa damu hiyo.

"Guys can donate to Kijabe Hospital at their Westlands branch, Azure Towers Lantana road - opposite Baptist church. Contact 0787145122. Thank you for showing concern as you whisper a prayer to God for her healing," aliongezea Veroonica