Mutahi Kagwe, Betty Maina: Sura Mpya katika serikali ya Uhuru

Waliopendekezwa kujiunga na baraza la mawaziri Betty Maina na Mutahi Kagwe.
Waliopendekezwa kujiunga na baraza la mawaziri Betty Maina na Mutahi Kagwe.
Mabadiliko yaliofanywa na rais Uhuru Kenyatta katika baraza lake la mawaziri yatamrejesha  Seneta wa zamani wa Nyri Mutahi Kagwe  serikalini endapo bunge litaidhinisha uteuzi wake . Katika mabadiliko hayo yaliytangazwa na Kenyatta akiwa  Mombasa ,Kagwe atahudumu katika wizara ya Afya  iliyokuwa ikishikilia wali na Sicily Kariuki ambaye sasa ndiye waziri wa maji .

Kati ya mwaka wa 2002 na 2007  Kagwe  alihudumu kama mbunge  wa tano wa eneo bunge la  Mukurweini . Kama mbunge  alikuwa mwenyekiti wa kamati ya bunge  kuhusu fedha ,biashara  ,utalii na mipango  kabla ya uteuzi wake kama waziri chini ya utawala wa  rais mstaafu Mwaki Kibaki . Kagwe baadaye alichaguliwa kuwa seneta wa kwanza wa Nyeri . Katika bunge la 11  alikuwa mwenyekiti wa kamati ya senate kuhusu ICT  na kuhudumu kama mwanachama wa kamati ya senate kuhusu  fedha na bajeti .Amewahi pia kuwa mwenyekiti wa kamati ya senate kuhusu Elimu .

Alipokuwa waziri , aliongoza ujenzi wa  mfumo maalum wa Kebo ya mtandao wa  East African Marine System – mradi mkubwa sana  na wa kipekee katika kanda ya afrika mashariki . Kagwe ndiy aliyefadhili mswada wa  usalama wa mtandaoni na ulinzi wad eta katika senate .Mwaka jana aliteuliwa na waziri wa kawi  Charles Keter  kuhudumu katika  tume ya uthibiti wa kawi na Petroli (EPRA).

Mwingine atakayejiunga na baraza la mawaziri la rais Kenyatta ni Betty Maina ambaye amekuwa akihudumu kama katibu wa kudumu wa  wizara ya Mazingira na Misitu . Ameteuliwa kuwa waziri mpya wa  Viwanda ,biashara na ustawi wa kibiashara . Maina pia amwahi kuhudumu kama katibu w akudumu wa  katika idara ya  uwekezaji na viwanda katika wizara ya viwanda na  vyama vya ushirika . Aliwahi kuhudumu kama afisa mkuu mtendaji wa muungano wa watengenezaji wa bidhaa (KAM). Awali aliwahi kuhudumu  katika nydhifa mbali mbali katika  Taasisi ya masuala ya kiuchumi ,Kituo cha kimatiafa cha  Biashara za kibinafsi  na katika taasisi ya Uongozi nchini Kenya .