Akizungumza katika mahojiano na Clouds Media akiwa na mke wake wa pili na wa tatu Mwaka amesema tama ndio iliyomfanya kuoa wanawake wengi Amesema alimuoa mke wake wa pili bila mke wake wa kwanza kujua lakini akapata ugumu kuendelea kuficha na hivyo basi akamtambua mke wake wa pili kwa wa kwanza . Mke wake wa pili amesema alifahamu kwamba mume wake alikuwa na mke wa kwanza lakini alikuwa na utulivu ili kufahamiana naye na baadaye wakazoaeana .
Mke wa pili amesema baadaye waligundua mume wao walikuwa na mwanamke wa tatu na wakadhani ni uhusiano ambao utapita lakini baadaye wakakubali kwamba mume wao alikuwa keshaoa mke wa tatu! .
" Wakati wa likizo tunapokutana kama familia ,mke mwenza aliniarifu kwamba uhusiano wa mume wetu na Yule mwanamke wa tatu umekuwa wa kudumu .Tulienda katika nyumba yake kumtafuta lakini hatukumpata ,tukachukua picha za mtoto wake na kuziweka katika status zetu za whatsapp ili kumjulisha mume wetu kwamba tumeigundua siri yake ‘. Amesema mke wake wa pili .
Mume naye aliamua kuziweka picha za wake zake wote watatu katika instagram ili kuzikabili picha za mke wake wa kwanza na wa pili jambo ambalo lilileta mgogoro hata zaidi . Mke wa pili anasema walitengana kwa muda lakini akakubali kukutana na mke wa tatu kwa sababu naye pia alipokelewa na mke wa kwanza .