Naibu Jaji Mkuu Mwilu aponea chupu chupu.

Mahakama kuu  imeamuru kwamba Naibu jaji mkuu Philomena Mwilu hatoshtakiwa  kwani ushahidi wa  DCI  dhidi yake ulipatikana  kwa njia inayokiuka sheria .

Jopo la majaji watano hivyo basi limefutilia mbali  kesi ya uhalifu dhidi yake  kutokana na jinsi ushahidi   huo  ulivyopatikana .

Majaji hata hivyo wamesema kulikuwa na msingi ufaao wa kisheria kumfungulia mashtaka .

  Idara za DCI na DPP zilikuwa zimemkabaa koo Mwilu  na kupendekeza mashtaka kadhaa dhidi yake ikiwemo kutumia vibaya maamlaka yake kutokana na  malipo aliyopokea kutoka kwa Benki iliyofilisika ya Imperial .

Kesi hiyo ilizua  tofauti kubwa kati ya idara hizo mbili na ile ya mahakama   kwani mtazamo wa wanaomwunga Mwilu mkono ulikuwa wa kuonewa kwa ajili ya msimamo wake wakati wa  kesi ya Kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais mwaka wa 2017 .