''Najua baba alitabasamu,''Kanze Dena amsifu dadake baada ya kupoteza baba

kanze
kanze
Msemi wa Ikulu ya Rais Bi Kanze Dena hajakuwa kwenye mtandao wa kijamii kwa muda mrefu.
Hata hivyo, ndoto ya dada yake mdogo Bi Elsie imeng'aa sana kwani binti huyu ameweza kuwa miongoni mwa washindi wa shindano la 'Mr and Miss World Kenya.
Elsie Stephen mwenye rinda la kijani kibichi.

Elsie Stephen dada yake Kanze aliweka picha yake kwenye mtandao wa kijamii na kuandika,

THIS WAS THE TOUGHEST BOOTCAMP YET THE MOST FULFILLING EXPERIENCE YET..BEING PART OF KENYA’S MOST PRESTIGIOUS PAGEANT WAS SUCH AN HONOUR. I AM NOW PART OF THE MWK FAMILY AND I MET AMAZING YOUNG AND VIBRANT CONTESTANTS WHO I ALREADY MISS.

Kanze Dena, dada yake Elsie naye akiwa na furaha na bashasha aliandika ujumbe mtamu kwenye mtandao wa kijamii na kusema kuwa, dada yao amefanya wajivunie sana kama familia na kusema kuwa, ana uhakika kuwa alipo marehemu baba yao,alitabasamu kwa sababu binti yake amekuwa mwanamke jasiri sana.

''YOU MADE US DO PROUD SIS..AND I KNOW DADDY SMILED.. HIS LITTLE GIRL HAS BECOME SUCH A STRONG AND CONFIDENT WOMAN. LOTS OF LOVE. #MUNGUMBELE,’ Kanze alisema.

Mabinti hawa walipoteza baba yao mwaka wa 2018 baada ya kupoteza mama yao mwaka wa 2007 baada ya kuugua na saratani ya utumbo mkubwa, 'Colon'.