NAVAKHOLO: Watu 17 Walazwa Hospitali Baada Ya Kula Chakula Kilichoharibika Katika Mazishi

picha: the-star.co.ke

Watu kumi na saba wanapokea matibabu katika hospitali ya Navakholo, kaunti ya Kakamega, baada ya kula chakula kilichokuwa kimeharibika katika hafla ya mazishi eneo la Kisembe.

Wasimamizi wa hospitali hiyo walisema chakula hicho kilikuwa kimekaa siku nyingi na kuliwa kikiwa baridi na hivyo basi wametupilia mbali hofu ya kuwa kilikuwa na sumu.

Ifuatayo na masimulizi ya miongoni mwa wale walioathirika na chakula hicho.